MNARA WA MLINZI—TOLEO LA FUNZO Januari 2018

Toleo hili lina makala za funzo za Februari 26 hadi Aprili 1, 2018.

WALIJITOA WENYEWE KWA HIARI

Walijitoa Wenyewe kwa Hiari​—Madagaska

Wajue baadhi ya wahubiri ambao wamejitoa wenyewe ili kusaidia kueneza ujumbe wa Ufalme kotekote nchini Madagaska.

“Yeye Humpa Nguvu Mtu Aliyechoka”

Kadiri mwisho unavyokaribia, tunatarajia kwamba mikazo ya maisha itaongezeka. Andiko la mwaka 2018 linatukumbusha tumtumaini Yehova ili tupate nguvu.

Ukumbusho Huwaunganisha Watu wa Mungu

Ukumbusho huimarisha umoja wa watu wa Mungu katika njia zipi? Ukumbusho utaadhimishwa kwa mara ya mwisho lini?

Kwa Nini Umpe Yule Aliye na Kila Kitu?

Njia moja ya kuonyesha kwamba tunampenda Mungu ni kumpatia vitu vyetu. Tunanufaikaje tunapomheshimu Yehova kwa vitu vyetu vyenye thamani?

Ni Upendo wa Aina Gani Unaoleta Furaha ya Kweli?

Upendo wa kimungu unatofautianaje na upendo unaotajwa kwenye 2 Timotheo 3:2-4? Jibu la swali hilo litatusaidia tupate furaha ya kweli na turidhike.

Tofauti Kati ya Watu Wanaomtumikia Yehova na Wasiomtumikia

Kuna tofauti gani kati ya tabia za watu wa siku za mwisho na sifa zinazoonyeshwa na watu wa Mungu?

Je, Wajua?

Je, kanuni zinazopatikana katika Sheria ya Musa zilitumiwa kutatua migogoro ya kila siku katika taifa la kale la Israeli?