Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Dokezo la Kujifunza

Dokezo la Kujifunza

Tanguliza Mambo Muhimu

Sisi sote hatuna muda mwingi wa kujifunza kibinafsi. Tunawezaje kutumia vizuri kabisa muda tunaopata? Kwanza, jifunze kwa mwendo wa taratibu. Utanufaika zaidi kwa kujifunza habari chache kwa makini kuliko kupitia haraka-haraka habari nyingi.

Kisha, utangulize mambo muhimu. (Efe. 5:15, 16) Fikiria mapendekezo yafuatayo:

  • Soma Biblia kila siku. (Zab. 1:2) Ratiba yetu ya kila juma ya usomaji wa Biblia kwa ajili ya mkutano wa katikati ya juma ni njia nzuri ya kuanza kusoma Biblia.

  • Tayarisha Funzo la Mnara wa Mlinzi na mkutano wa katikati ya juma. Uwe tayari kutoa maelezo.​—Zab. 22:22.

  • Pia kulingana na muda ulio nao jitahidi kuchunguza habari nyingine za kiroho, kama vile magazeti yetu ya watu wote, video, na habari zilizochapishwa kwenye jw.org.

  • Uwe na mradi wa kujifunza. Unaweza kufanya utafiti kuhusu changamoto unayokabili, swali unalojiuliza, au habari ya Biblia ambayo ungependa kuielewa vizuri. Ili kupata madokezo, chunguza sehemu ya “Mazoezi ya Kujifunza Biblia” kwenye jw.org.