Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wafalme Wanaopingana Katika Wakati wa Mwisho

Wafalme Wanaopingana Katika Wakati wa Mwisho

Baadhi ya unabii unaotajwa kwenye chati hii unafafanua matukio yanayotendeka katika kipindi kilekile cha wakati. Unabii huo unatoa uthibitisho mbalimbali kwamba tunaishi katika “wakati wa mwisho.”—Dan. 12:4.

  • Maandiko Ufu. 11:7; 12:13, 17; 13:1-8, 12

    Unabii “Mnyama wa mwituni” amewatawala watu duniani kwa zaidi ya miaka 3,000. Katika wakati wa mwisho, kichwa chake cha saba kinajeruhiwa. Baadaye, kichwa hicho kinapona na “dunia yote” inamfuata mnyama huyo. Shetani anamtumia mnyama huyo wa mwituni “kupigana na wale waliobaki.”

    Utimizo Baada ya Gharika, serikali za wanadamu zinazompinga Yehova zajitokeza. Karne nyingi baadaye, wakati wa Vita vya Kwanza vya Ulimwengu, Milki ya Uingereza inadhoofika sana. Inapata nguvu tena inapoungana na Marekani. Katika wakati wa mwisho, Shetani amekuwa akitumia mfumo wake wote wa kisiasa kuwatesa watu wa Mungu.

  • Andiko Dan. 11:25-45

    Unabii Mapambano kati ya mfalme wa kaskazini na mfalme wa kusini katika wakati wa mwisho.

    Utimizo Serikali ya Ujerumani na ile Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani zapambana. Katika mwaka wa 1945 Muungano wa Sovieti na nchi zinazouunga mkono zinakuwa mfalme wa kaskazini. Mwaka wa 1991, Muungano wa Sovieti unavunjika, na baadaye, serikali ya Urusi na nchi zinazoiunga mkono zinakuwa mfalme wa kaskazini.

  • Maandiko Isa. 61:1; Mal. 3:1; Luka 4:18

    Unabii Yehova anamtuma “mjumbe” wake ili ‘afungue njia’ kabla ya Ufalme wa Kimasihi kusimamishwa. “Mjumbe” huyo anaanza ‘kuwatangazia wapole habari njema.’

    Utimizo Kuanzia mwaka wa 1870 na kuendelea, C. T. Russell na wenzake wanajifunza Biblia kwa bidii ili wafafanue mafundisho ya kweli. Katika miaka ya 1880, wanaanza kukazia kwamba watumishi wa Mungu wanapaswa kuhubiri. Wanachapisha makala kama vile “Wahubiri 1,000 Wanahitajika” na “Walitiwa Mafuta Ili Kuhubiri.”

  • Andiko Mt. 13:24-30, 36-43

    Unabii Adui anapanda magugu katika shamba la ngano, na magugu hayo yanaachwa yaendelee kukua, nayo yanaficha ngano hadi kipindi cha mavuno kitakapofika; kisha magugu yanatenganishwa na ngano.

    Utimizo Kuanzia mwaka wa 1870 na kuendelea, tofauti kati ya Wakristo wa kweli na wa uwongo inazidi kuwa wazi. Katika wakati wa mwisho, Wakristo wa kweli wanakusanywa na kutenganishwa na Wakristo wa uwongo.

  • Andiko Dan. 2:31-33, 41-43

    Unabii Miguu ya chuma na udongo ni sehemu ya sanamu iliyotengenezwa kwa madini mbalimbali.

    Utimizo Udongo unafananisha watu wanaotawaliwa na Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani ambao wanapinga utawala wa serikali hiyo. Watu hao wanadhoofisha uwezo wa serikali hiyo ya ulimwengu wa kutumia nguvu zake kikamili kama chuma.

  • Maandiko Mt. 13:30; 24:14, 45; 28:19, 20

    Unabii “Ngano” inakusanywa “ghalani,” na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” anawekwa rasmi ili asimamie “watumishi wa nyumbani.” Kazi ya kuhubiri “habari njema ya Ufalme” inaanza kuenea katika “dunia yote inayokaliwa.”

    Utimizo Mwaka wa 1919 mtumwa mwaminifu anawekwa rasmi ili awasimamie watu wa Mungu. Kuanzia wakati huo na kuendelea, Wanafunzi wa Biblia wamekuwa wakihubiri zaidi na zaidi. Leo, Mashahidi wa Yehova wanahubiri katika nchi zaidi ya 200 na wanachapisha machapisho yanayotegemea Biblia katika lugha zaidi ya 1,000.

  • Maandiko Dan. 12:11; Ufu. 13:11, 14, 15

    Unabii Mnyama wa mwituni mwenye pembe mbili anawaambia watu duniani watengeneze “sanamu ya yule mnyama wa mwituni” na anaipa ‘pumzi sanamu hiyo.’

    Utimizo Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani yawa mstari wa mbele katika kuanzisha Ushirika wa Mataifa. Ushirika huo unaungwa mkono na mataifa mengine. Hatimaye, mfalme wa kaskazini anajiunga na Ushirika huo pia—lakini anafanya hivyo kuanzia mwaka wa 1926 hadi 1933 tu. Kama ilivyo kwa Umoja wa Mataifa (UM) leo, Ushirika huo unasifiwa kwamba unaweza kutimiza mambo yanayoweza tu kutimizwa na Ufalme wa Mungu.

  • Andiko Dan. 8:23, 24

    Unabii Mfalme mwenye uso mkali analeta “uharibifu kwa njia isiyo ya kawaida.”

    Utimizo Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani imesababisha uharibifu mkubwa sana. Kwa mfano, wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu, Marekani ilisababisha uharibifu ambao haujawahi kuonekana kamwe ilipomwangushia adui yake mabomu mawili ya atomu.

  • Maandiko Dan. 11:31; Ufu. 17:3, 7-11

    Unabii Mnyama wa mwituni mwenye “rangi nyekundu” na pembe kumi anapanda kutoka katika shimo refu lisilo na mwisho, naye ni mfalme wa nane. Kitabu cha Danieli kinamtaja mfalme huyo wa nane kuwa, “kile kitu chenye kuchukiza sana kinachosababisha ukiwa.”

    Utimizo Ushirika wa Mataifa unaingia katika kipindi cha kutotenda wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu. Baada ya vita, UM ‘unasimamishwa.’ Kama ilivyokuwa kwa Ushirika wa Mataifa, UM unapewa utukufu ambao Ufalme wa Mungu unapaswa kupewa. UM utashambulia dini.

  • Maandiko 1 The. 5:3; Ufu. 17:16

    Unabii Mataifa yanatangaza “amani na usalama,” kisha “zile pembe kumi” na “yule mnyama wa mwituni” wanamshambulia “yule kahaba” na kumwangamiza. Baada ya hapo, mataifa yanaharibiwa.

    Utimizo Mataifa yatadai kwamba yamefanikiwa kupata amani na usalama. Kisha, mataifa yanayounga mkono UM yataharibu mashirika ya dini ya uwongo. Huo utakuwa mwanzo wa dhiki kuu. Dhiki hiyo itakwisha wakati mfumo wote wa ulimwengu utakapoharibiwa katika vita vya Har–Magedoni.

  • Maandiko Eze. 38:11, 14-17; Mt. 24:31

    Unabii Gogu ashambulia nchi ya watu wa Mungu. Kisha, malaika wanawakusanya wale “waliochaguliwa.”

    Utimizo Mfalme wa kaskazini, pamoja na serikali nyingine za ulimwengu, zitawashambulia watu wa Mungu. Wakati fulani baada ya shambulizi hilo kuanza, watiwa-mafuta waliobaki watakusanywa kwenda mbinguni.

  • Maandiko Eze. 38:18-23; Dan. 2:34, 35, 44, 45; Ufu. 6:2; 16:14, 16; 17:14; 19:20

    Unabii “Yule aliyeketi” juu ya “farasi mweupe” anakamilisha “ushindi wake” kwa kumharibu Gogu na jeshi lake. “Yule mnyama wa mwituni” ‘anatupwa ndani ya ziwa la moto,’ na sanamu ile kubwa inapondwapondwa.

    Utimizo Yesu, Mfalme anayetawala wa Ufalme wa Mungu anawaokoa watu wa Mungu. Akiwa pamoja na watawala wenzake 144,000 na majeshi ya malaika, Yesu anauharibu muungano wa mataifa, yaani, mfumo wote wa kisiasa wa Shetani.