MNARA WA MLINZI—TOLEO LA FUNZO Septemba 2019

Toleo hili lina makala za funzo za Oktoba 28–Desemba 1, 2019.

Yehova Anawathamini Watumishi Wake Wanyenyekevu

Unyenyekevu ni mojawapo ya sifa muhimu zaidi tunazohitaji kusitawisha. Mabadiliko maishani yanaweza kujaribu unyenyekevu wetu jinsi gani?

Har–Magedoni Ni Habari Njema!

Ni matukio gani makubwa yatakayotangulia Har–Magedoni? Tunaweza kuendeleaje kuwa waaminifu kadiri mwisho unavyokaribia?

Jitiishe kwa Yehova kwa Hiari—Kwa Nini na Jinsi Gani?

Wazee wa kutaniko, akina baba, na akina mama wanaweza kujifunza kuhusu kujitiisha kutokana na mfano wa Gavana Nehemia; Mfalme Daudi; na Maria, mama ya Yesu.

“Njooni Kwangu, . . . Nami Nitawaburudisha”

Kukubali mwaliko wa Yesu kunahusisha nini? Tutaendelea kupata burudisho chini ya nira ya Yesu ikiwa tutafanya mambo matatu.

“Tazama! Umati Mkubwa”

Katika maono ya kinabii ya Yohana, Yehova alitambulisha “umati mkubwa,” ukubwa wake, na watu mbalimbali wanaofanyiza umati huo ambao ungeokoka dhiki kuu na kuishi milele duniani.