Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Watu Waliokufa Wataishi Tena?

Je, Watu Waliokufa Wataishi Tena?

Kila mmoja wetu ameathiriwa na kifo. Lakini je, kifo ndio mwisho wa mambo yote? Je, watu waliokufa wamesahaulika kabisa? Je, wataishi tena?

BIBLIA INASEMA:

WATU WALIOKUFA HAWAJASAHAULIKA

“Wote walio katika makaburi ya ukumbusho . . . [watatoka].”​—Yohana 5:28, 29.

Mungu anawakumbuka watu waliokufa; wale walio kwenye kumbukumbu yake wataishi tena.

KUTAKUWA NA UFUFUO HAPA DUNIANI

“Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.”​—Matendo 24:15.

Mabilioni ya watu watarudishiwa uhai wakiwa na tumaini la kuishi milele katika dunia iliyojaa amani.

TUMAINI LA UFUFUO NI LA HAKIKA

“[Mungu] huhesabu idadi ya nyota; zote anaziita kwa majina.”—Zaburi 147:4.

Kwa kuwa Mungu anajua majina ya nyota zote, bila shaka ni rahisi kwake kuwakumbuka watu ambao atawafufua.