Je, Watu Waliokufa Wataishi Tena?
Kila mmoja wetu ameathiriwa na kifo. Lakini je, kifo ndio mwisho wa mambo yote? Je, watu waliokufa wamesahaulika kabisa? Je, wataishi tena?
BIBLIA INASEMA:
WATU WALIOKUFA HAWAJASAHAULIKA
“Wote walio katika makaburi ya ukumbusho . . . [watatoka].”—Yohana 5:28, 29.
Mungu anawakumbuka watu waliokufa; wale walio kwenye kumbukumbu yake wataishi tena.
KUTAKUWA NA UFUFUO HAPA DUNIANI
“Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.”—Matendo 24:15.
Mabilioni ya watu watarudishiwa uhai wakiwa na tumaini la kuishi milele katika dunia iliyojaa amani.
TUMAINI LA UFUFUO NI LA HAKIKA
“[Mungu] huhesabu idadi ya nyota; zote anaziita kwa majina.”—Zaburi 147:4.
Kwa kuwa Mungu anajua majina ya nyota zote, bila shaka ni rahisi kwake kuwakumbuka watu ambao atawafufua.