Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Sehemu ya kitabu cha Isaya kutoka kwenye Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi kilicho pamoja na tafsiri ya kitabu cha Isaya katika Kiarabu. Ujumbe wa Neno la Mungu haubadiliki

Je, Neno la Mungu Limebadilishwa?

Je, Neno la Mungu Limebadilishwa?

Baadhi ya watu wanafikiri kwamba Neno la Mungu limebadilishwa. Nabii Isaya aliandika kwamba neno la Mungu “linadumu milele.” (Isaya 40:8) Tunawezaje kuwa na uhakika kwamba Neno la Mungu ni sahihi?

Mungu ana uwezo wa kuhakikisha kwamba Neno lake linatunzwa na kubaki likiwa sahihi. Kwa mfano, katika nyakati za kale, wanakili walionakili Neno la Mungu, walihakikisha wanahesabu kila herufi ili neno lolote lisiongezwe, kubadilishwa au kuondolewa. Hata hivyo, kwa kuwa wanadamu si wakamilifu, baadhi ya wanakili walifanya makosa madogo-madogo ambayo hayakubadili ujumbe wa awali.

TUNAWEZAJE KUWA NA UHAKIKA KWAMBA MAANDIKO MATAKATIFU HAYAJABADILISHWA?

Kuna maelfu ya hati za kale za Maandiko Matakatifu. Ikiwa hati moja ina tofauti hata ndogo, inaweza kulinganishwa na hati nyingine nyingi ili kupata ukweli.—Ili kupata habari zaidi, soma makala yenye kichwa, “Je, Biblia Imebadilishwa au Kupotoshwa?” kwenye jw.org/sw.

Kwa mfano, fikiria hati za kale zinazoitwa Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi, vilivyogunduliwa kwenye mapango karibu na Bahari ya Chumvi mwaka wa 1947. Hati hizo za kale ambazo zina baadhi ya vitabu vya Maandiko Matakatifu zimekuwepo kwa zaidi ya miaka elfu mbili. Wasomi walilinganisha vitabu hivyo vya kukunjwa vya kale na Maandiko Matakatifu tuliyonayo leo. Waligundua nini?

Wasomi waligundua kwamba ujumbe unaopatikana katika Neno la Mungu leo, unafanana na ujumbe ulio katika hati hizo za kale. * Jambo hilo linatuthibitishia kwamba, ujumbe tunaosoma leo katika Maandiko Matakatifu ni uleule ambao Mungu aliusema zamani. Tuna uhakika kwamba Mungu aliyatunza Maandiko Matakatifu yakiwa sahihi kwa ajili yetu leo.

Kwa hiyo, tunaweza kusoma Neno la Mungu tukiwa na uhakika kabisa kwamba ni ujumbe sahihi kutoka kwa Mungu. Tukiwa na hilo akilini, acheni tuone mambo tunayoweza kujifunza kumhusu Mungu kupitia manabii wake.

^ fu. 7 The Complete Dead Sea Scrolls in English, cha Geza Vermes, ukurasa wa 16.