Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, unaweza kuwasaidia wengine licha ya umri wao, taifa lao, au dini yao?

Watu Wanaowasaidia Wengine Hupata Baraka

Watu Wanaowasaidia Wengine Hupata Baraka

Watu wengi ulimwenguni hawana uwezo wa kupata chakula na makazi. Wengine hawana tumaini la wakati ujao. Tukijitahidi kuwasaidia watu wenye shida tutapata kibali cha Mungu na baraka zake.

MAANDIKO MATAKATIFU YANASEMA NINI?

“Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova, Naye Atamlipa kwa anayotenda.”​—METHALI 19:17.

KUMSAIDIA MTU MWENYE SHIDA KUNAHUSISHA NINI?

Yesu alisimulia kuhusu mwanamume fulani ambaye alishambuliwa na wezi njiani na aliachwa hapo akiwa karibu kufa. (Luka 10:29-37) Lakini mwanamume fulani mgeni akasimama na kumtibu majeraha yake. Alimsaidia mwanamume huyo licha ya kwamba tamaduni zao zilitofautiana.

Mwanamume huyo mwenye fadhili hakumpa tu huduma ya kwanza na vitu alivyohitaji bali pia alimfariji na kumsaidia kupata kitulizo kutokana na hali aliyokabili.

Tunajifunza nini katika simulizi hili? Yesu alionyesha kwamba tunapaswa kuwasaidia watu wenye matatizo kadiri tuwezavyo. (Methali 14:31) Maandiko Matakatifu yanafundisha kwamba, hivi karibuni Mungu ataondoa umaskini na kuteseka. Huenda tukajiuliza, Mungu atatimiza mambo hayo lini na jinsi gani? Makala inayofuata itazungumzia baraka ambazo Muumba wetu mwenye upendo atatupatia wakati ujao.