Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Sala Zinaweza Kukusaidiaje?

Sala Zinaweza Kukusaidiaje?

Pamela aliyekuwa na ugonjwa wa kansa alitafuta matibabu. Hata hivyo, alisali pia kwa Mungu ili ampe nguvu za kuvumilia ugonjwa huo. Je, kusali kwa Mungu kulimsaidia?

Pamela anasema: “Nilipokuwa nikipata matibabu ya kansa, mara nyingi niliogopa sana. Lakini niliposali kwa Yehova Mungu, nilihisi utulivu na nikaanza kufikiria mambo kwa njia nzuri. Bado ninapata maumivu makali sana lakini sala inanisaidia kudumisha mtazamo unaofaa. Watu wanaponiuliza ninahisije, ninawaambia, ‘Bado nina maumivu, lakini nina furaha!’”

Bila shaka, hatuhitaji kusubiri hadi tuwe na tatizo kubwa la afya au matatizo mengine ili tusali. Sisi sote tunakabili changamoto, kubwa na ndogo, na mara nyingi tunahisi tunahitaji msaada ili kukabiliana nazo. Je, sala zinaweza kutusaidia?

Biblia inasema: “Mtupie Yehova mzigo wako, naye atakutegemeza. Hataruhusu kamwe mwadilifu aanguke.” (Zaburi 55:22) Maneno hayo yanafariji sana. Hivyo, sala zinaweza kukusaidia kwa njia gani? Unaposali kwa Mungu kwa njia inayofaa, atakupatia kile unachohitaji ili ukabiliane na changamoto ulizo nazo.​—Ona sanduku “ Unaweza Kunufaikaje kwa Kusali?