Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umesoma kwa makini matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:

Kwa nini Yehova aliwaruhusu Waisraeli wapigane?

Yehova ni mwenye upendo. Hata hivyo, nyakati fulani aliwaruhusu wapigane wakati uovu na ukandamizaji ulipotishia watu wake. Ni Mungu peke yake aliyeamua ni nani angepigana vita na angepigana lini.—w15 11/1, ukurasa wa 4-5.

Ni mambo gani muhimu ambayo wazazi wanaweza kufanya ili kuwazoeza vijana wao wamtumikie Yehova?

Wazazi wanapaswa kuwapenda watoto wao na kuonyesha unyenyekevu kwa matendo. Pia ni muhimu wazazi kuonyesha ufahamu na kujitahidi kuelewa watoto wao.—w15 11/15, ukurasa wa 9-11.

Kwa nini papa hapaswi kuonwa kuwa mrithi wa Petro?

Andiko la Mathayo 16:17, 18 halisemi kwamba mtume Petro angekuwa kichwa cha kutaniko la Kikristo. Biblia inaonyesha kwamba Petro hakupewa uongozi, bali Yesu ndiye aliyepaswa kuwa jiwe la pembeni la msingi la kutaniko. (1 Pet. 2:4-8)—w15 12/1, ukurasa wa 12-14.

Tunapaswa kufikiria mambo gani kabla ya kuzungumza?

Ili kutumia ulimi wetu vizuri, tunapaswa kuzingatia (1) wakati unaofaa wa kusema (Mhu. 3:7), (2) maneno yanayofaa (Met. 12:18), na (3) jinsi ya kuzungumza (Met. 25:15).—w15 12/15, ukurasa wa 19-22.

Wakristo wanapaswa kuepuka mambo gani yasiyo ya unyoofu?

Wakristo wa kweli huepuka kuwadanganya na kuwachongea wengine. Hawadanganyi au kuwachongea wengine ili kuwaharibia sifa, pia hawawalaghai wengine wala kuiba.—wp16.1, ukurasa wa 5.

“Wakuu wa makuhani” wanaotajwa katika Biblia ni nani?

Inaonekana maneno “wakuu wa makuhani” yanarejelea washiriki wakuu wa ukuhani, ambao walitia ndani makuhani wakuu wa zamani walioondolewa katika vyeo vyao.—wp16.1, ukurasa wa 10.

Tunapaswa kumtendeaje mtu anayekula mkate na kunywa divai wakati wa Ukumbusho?

Wakristo hawawainui watu kama hao. Mtu ambaye ametiwa mafuta kikweli hangependa kuinuliwa; wala kutumia mwito aliopewa na Mungu kujitambulisha kwa wengine. (Mt. 23:8-12)—w16.01, ukurasa wa 23-24.

Tunaweza kujifunza nini kutokana na jinsi Abrahamu alivyokuwa rafiki ya Mungu?

Huenda Abrahamu alijifunza kumhusu Mungu kutoka kwa Shemu. Na Abrahamu alipata uzoefu kutokana na jinsi Mungu alivyoshughulika naye na familia yake. Tunaweza kujitahidi kumwiga.—w16.02, ukurasa wa 9-10.

Ni nani walioweka sura na mistari ya Biblia?

Kasisi Stephen Langton aliyeishi katika karne ya 13 ndiye aliyeigawa Biblia katika sura. Waandishi Wayahudi walikuwa wamegawa Maandiko ya Kiebrania katika mistari, naye msomi Robert Estienne aliyeishi katika karne ya 16 akafanya vivyo hivyo na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.—wp16.2, ukurasa wa 14-15.

Je, Shetani alimchukua Yesu kihalisi na kumpeleka hekaluni alipokuwa akimshawishi?

Hatuna uhakika. Huenda andiko la Mathayo 4:5 na Luka 4:9 linamaanisha kwamba Yesu aliona maono au kwamba alisimama kwenye sehemu ya juu katika eneo la hekalu.—w16.03, ukurasa wa 31-32.

Huduma yetu ya Kikristo ni kama umande katika njia gani?

Umande hufanyizwa pole kwa pole, huburudisha na huendeleza uhai. Umande halisi ni baraka kutoka kwa Mungu. (Kum. 33:13) Jitihada za pamoja za watu wa Mungu katika huduma hufanana na umande.—w16.04, ukurasa wa 4.