Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Darasa la 108 la Gileadi Lahimizwa Kutoa Utumishi Mtakatifu

Darasa la 108 la Gileadi Lahimizwa Kutoa Utumishi Mtakatifu

Darasa la 108 la Gileadi Lahimizwa Kutoa Utumishi Mtakatifu

KATIKA Biblia, ibada ya Mungu mara nyingi huitwa “utumishi mtakatifu.” Msemo huo hutokana na neno la Kigiriki linalorejezea kutoa utumishi mtakatifu kwa Mungu. (Waroma 9:4) Watu 5,562 waliosikiliza programu ya kuhitimu kwa darasa la 108 la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower walisikia wasemaji wakitoa ushauri wenye kutumika ambao ungewasaidia wahitimu watoe utumishi mtakatifu unaokubalika kwa Yehova Mungu. *

Mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova, Theodore Jaracz, alikuwa mwenyekiti. Programu hiyo ilifunguliwa kwa wimbo nambari 52, “Jina la Baba Yetu.” Ubeti wa pili wa wimbo huo husema hivi: “Twatafuta njia za kutakasa jina lako.” Wimbo huo kwa kweli ulionyesha tamaa ya kutoka moyoni ya wanafunzi wa darasa lenye kuhitimu (waliotoka katika nchi 10) ya kutumia mazoezi yao katika migawo yao ya umishonari, ambayo ingekuwa katika nchi mbalimbali 17.

Katika maneno yake ya kufungua, Ndugu Jaracz alivuta uangalifu kwenye miezi mitano ambayo wanafunzi walitumia kujifunza Biblia kwa kina, jambo lililowatayarisha kutumikia katika maeneo ya kigeni. Hilo liliwasaidia ‘kuhakikisha mambo yote,’ yaani, kuchanganua yale waliyokuwa wamejifunza kwa kuyalinganisha na Neno la Mungu, na ‘kushika sana lililo bora.’ (1 Wathesalonike 5:21) Aliwatia moyo wawe waaminifu kwa Yehova, kwa Neno lake, na kwa migawo waliyozoezwa. Ni nini kitakachowasaidia wafanyapo yote hayo?

Ushauri Unaofaa Katika Kutoa Utumishi Mtakatifu

Lon Schilling, mshiriki wa Halmashauri ya Utendaji wa Betheli, aliongea juu ya kichwa “Je, Utapita Mtihani wa Kuwa Mtu Mwenye Kukubali Sababu?” Alikazia manufaa ya kuwa mwenye kukubali sababu, jambo linaloonyesha hekima ya kimungu. (Yakobo 3:17) Kukubali sababu hutia ndani kuwa mwenye kunyumbulika, kuwa bila ubaguzi, mwenye kiasi, mwenye ufikirio, na mwenye kuvumilia. “Watu wenye kukubali sababu ni wenye usawaziko wanaposhughulika na wengine. Hawapiti kiasi,” akasema Ndugu Schilling. Ni nini kinachoweza kumsaidia mishonari awe mwenye kukubali sababu? Kuwa na maoni yaliyosawazika kujihusu, kujinufaisha na fursa za kusikiliza na kujifunza kutoka kwa wengine, na kuwa tayari kufikiria maoni ya wengine bila kuridhia viwango vya kimungu.—1 Wakorintho 9:19-23.

“Usisahau Kula!” ndicho kilichokuwa kichwa chenye kuvutia cha sehemu iliyofuata kwenye programu, ambayo ilitolewa na Samuel Herd, mshiriki mwingine wa Baraza Linaloongoza. Alikazia thamani ya kula vizuri kiroho ili mtu aendelee kuwa na nguvu za kutoa utumishi mtakatifu. “Upesi, utendaji wako wa kiroho utaongezeka unapoanza mgawo wako wa kuhubiri na kufundisha,” Ndugu Herd akasema. “Kwa hiyo, kutakuwa na uhitaji wa kuongeza ulaji wako wa chakula cha kiroho ili usawazishe nguvu zako.” Kula chakula cha kiroho kwa ukawaida kunaweza kumsaidia mishonari aepuke udhaifu wa kiroho na vilevile tamaa ya kurudi nyumbani. Huchangia kuwa na uradhi na azimio la kubaki katika eneo lako la utumishi mtakatifu.—Wafilipi 4:13.

Mfunzi mmoja wa Gileadi, Lawrence Bowen, aliwatia moyo wanafunzi wenye kuhitimu ‘Warudie Chanzo.’ Alimaanisha nini? Aliwaomba wote waliohudhuria wafungue Mithali 1:7, ambayo husema: “Kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa [“ujuzi,” NW].” Msemaji huyo alieleza hivi: “Ujuzi wowote ambao hupuuza ukweli muhimu wa kuwapo kwa Yehova kwa kweli hauwezi kuwa ujuzi wa kweli wala kutokeza uelewevu unaofaa.” Ndugu Bowen alilinganisha Neno la Mungu, Biblia na vipande vya mchezo wa fumbo. Vipande hivyo vinapowekwa pamoja, picha hutokea. Kadiri vipande vinapokuwa vingi, ndivyo picha inavyokuwa kubwa na wazi na ndivyo mtu anavyoithamini zaidi. Hilo laweza kusaidia wote watoe utumishi mtakatifu kwa Mungu.

Wallace Liverance, msajili wa Shule ya Gileadi, alimalizia mfululizo huo wa hotuba. Kichwa cha hotuba yake kilikuwa “Toa Shukrani Zikiwa Dhabihu Yako kwa Mungu.” Alivuta fikira kwenye simulizi la Yesu la kuponya wakoma kumi. (Luka 17:11-19) Ni mmoja tu aliyerudi kumsifu Mungu na kumshukuru Yesu. “Bila shaka, wale wengine walifurahi kuwa safi. Walipendezwa na hali yao safi, lakini yaonekana walichotaka tu ni kutambulishwa na kuhani kuwa safi,” akaeleza Ndugu Liverance. Kutakaswa kiroho kunakotokana na kujifunza kweli, pamoja na shukrani, kwapaswa kuchochea mtu aonyeshe shukrani kwa Mungu kwa wema wake. Wanafunzi wa darasa la 108 la Gileadi walitiwa moyo kutafakari matendo na wema wote wa Mungu ili wafanye utumishi wao na kujitolea kwao kuwe wonyesho wa shukrani kwa Mungu.—Zaburi 50:14, 23; 116:12, 17.

Mambo Yaliyoonwa na Mahojiano ya Jinsi ya Kufanya Hivyo

Mark Noumair, mfunzi mwingine wa Gileadi, alizungumzia sehemu iliyofuata ya programu. Alishughulika na mambo yaliyoonwa ya utumishi wa shambani ya darasa hilo wakati wa kipindi chao cha mazoezi. Wanafunzi walikuwa wametumia wastani wa miaka 12 hivi katika huduma ya wakati wote kabla ya kuja Gileadi. Wakiwa shuleni, walianzisha mafunzo mengi ya Biblia pamoja na watu wa malezi mbalimbali, kuonyesha kwamba wanafunzi hao walijua jinsi ya “kuwa mambo yote kwa watu wa namna zote.”—1 Wakorintho 9:22.

Baada ya wanafunzi kutoa mambo yaliyoonwa, Charles Molohan na William Samuelson walihoji baadhi ya washiriki wa familia ya Betheli na waangalizi wasafirio ambao walipata kuhudhuria shule ya Gileadi. Kati ya ndugu waliohojiwa, Robert Pevy, alitumikia huko Filipino baada ya kuhitimu kutoka katika darasa la 51 la Gileadi. Alikumbusha darasa hilo hivi: “Kunapokuwa na tatizo, kila mtu hutoa dokezo la jinsi ya kulitatua. Sikuzote kuna mtu stadi kukushinda, mtu atakayetoa dokezo bora zaidi. Lakini ukiichunguza Biblia na kujaribu kupata maoni ya Mungu kuhusu mambo, hakuna atakayeyashinda. Sikuzote hayo yatakuwa ndiyo maoni sahihi.”

Kwa kumalizia programu hiyo nzuri ya kiroho, John Barr, mshiriki wa Baraza Linaloongoza, aliongea juu ya kichwa “Toa Utumishi Mtakatifu Unaokubalika kwa Yehova.” Alionyesha jinsi utumishi mtakatifu uwezavyo kuonekana dhahiri katika huduma ya shambani ili kusaidia watu wenye mioyo minyoofu wamwabudu Mungu katika njia yenye kukubalika. Baada ya kusoma maneno ya Yesu kwenye Mathayo 4:10, Ndugu Barr alisema, “Ili tumwabudu Yehova pekee, lazima tuepuke aina zote zenye hila za ibada ya sanamu, kama vile kutamani, tamaa ya mali, na kujipendekeza. Inatufurahisha kama nini kufikiria kwamba kwa miaka mingi, tangu miaka ya mapema ya 1940, wamishonari wetu wamesitawisha rekodi bora kuhusu jambo hilo! Nasi tuna uhakika kwamba nyinyi wahitimu wa darasa la 108 la Gileadi mtafuata kielelezo chao chema. Mtatoa utumishi mtakatifu kwa Yehova, ambaye ni yeye pekee anayestahili kuupokea.”

Huo ulikuwa umalizio mzuri kwa programu yenye kujenga. Kisha kukawa na wakati wa kusikiliza salamu kutoka kwa watu waliowatakia mema kutoka sehemu mbalimbali za ulimwengu, wakati wa kutolewa kwa diploma, na wakati wa kusoma barua kutoka kwa wanadarasa, wakishukuru kwa mazoezi waliyopokea. Darasa lenye kuhitimu lilisihiwa lionyeshe sifa ya kutoacha migawo yao na utumishi wao kwa Yehova. Wahudhuriaji wote kutia ndani wageni kutoka katika nchi 25, walishiriki katika wimbo na sala ya kumalizia programu.

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 2 Programu hiyo ya Machi 11, 2000, ilitolewa katika Kituo cha Elimu cha Watchtower huko Patterson, New York.

[Sanduku katika ukurasa wa 23]

TAKWIMU ZA DARASA

Idadi ya nchi zilizowakilishwa: 10

Idadi ya nchi walikogawiwa: 17

Idadi ya wanafunzi: 46

Wastani wa umri: 34

Wastani wa miaka katika kweli: 16

Wastani wa miaka katika huduma ya wakati wote: 12

[Picha katika ukurasa wa 24]

Darasa la 108 Lililohitimu la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower

Katika orodha iliyo chini, nambari za safu zaanzia mbele kuelekea nyuma, na majina yameorodheshwa kuanzia kushoto kuelekea kulia katika kila safu.

(1) Amadori, E.; Cook, O; Byrne, M.; Lee, A. (2) Newsome, D.; Pederzolli, A.; Bigras, H.; Kato, T.; Gatewood, D. (3) Eade, D.; Eade, J.; Wells, S.; Jamison, J.; Gonzales, M.; Gonzales, J. (4) Kato, T.; Lohn, D.; Niklaus, Y.; Preiss, S.; Foster, P.; Ibarra, J. (5) Amadori, M.; Manning, M.; James, M.; Boström, A.; Gatewood, B.; Newsome, D. (6) Foster, B.; Jamison, R.; Hifinger, A.; Koffel, C.; Koffel, T.; Byrne, G (7) Hifinger, K.; Manning, C.; Cook, J.; Boström, J.; Lohn, E.; Pederzolli, A. (8) James, A.; Wells, L.; Preiss, D.; Niklaus, E.; Lee, M.; Ibarra, P.; Bigras, Y.