Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Vita Dhidi ya Umaskini Je, Ni Jambo Lisiloweza Kufanikiwa?

Vita Dhidi ya Umaskini Je, Ni Jambo Lisiloweza Kufanikiwa?

Vita Dhidi ya Umaskini Je, Ni Jambo Lisiloweza Kufanikiwa?

WATALII wanaozuru Umoja wa Mataifa huko New York City, huona jengo la Shirikisho la Kiuchumi na Kijamii, likiwa na mabomba na waya kwenye dari juu ya nyumba ya umma. Mwenye kutembeza watu aeleza: “Paa ‘lisilokamilika’ huonekana kwa kawaida kuwa ishara ya kikumbusha kwamba kazi ya kiuchumi na ya kijamii ya Umoja wa Mataifa haiishi kamwe; sikuzote kutakuwa na jambo zaidi la kufanywa ili kuboresha hali za maisha za watu ulimwenguni.”

Ijapokuwa Shirikisho hilo limejitolea kuchochea kiwango cha juu cha maisha, kazi hiyo yaonekana nyingi mno. Jambo lenye kupendeza ni kwamba, wakati wa huduma ya Yesu Kristo duniani katika karne ya kwanza W.K., alisema hivi: “Roho ya Yehova iko juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kutangaza habari njema kwa walio maskini.” (Luka 4:18) “Habari njema” alizotangaza ni zipi? Zilikuwa ujumbe unaohusu Ufalme ambao Yehova Mungu, yeye ambaye huwa “ngome ya maskini . . . katika dhiki,” atausimamisha Yesu Kristo akiwa Mfalme. Ufalme huo utatimiza nini? Isaya alitabiri: “BWANA wa majeshi atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, karamu ya vinono vilivyojaa mafuta, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, iliyochujwa sana. Amemeza mauti hata milele; na Bwana MUNGU atafuta machozi katika nyuso zote.”—Isaya 25:4-6, 8.

Je, ungependa kujua mengi kuhusu jinsi Ufalme wa Mungu “[utakavyo] boresha hali za maisha za watu ulimwenguni,” ili kusiwe na upungufu tena? Ona maelezo yaliyo chini ili upate kujua jinsi unavyoweza kupata kutembelewa na mwalimu anayestahili kukuonyesha mengi zaidi kuhusu yale ambayo Biblia husema juu ya mambo hayo.