Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Cheti cha Huduma Bora

Cheti cha Huduma Bora

Cheti cha Huduma Bora

HIRIKA la Maendeleo la Waandishi wa Habari wa Kongo na Afrika (AJOCAD) katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, hutoa cheti hicho kama “tunu kwa watu na mashirika ya kijamii yanayojipatia sifa kwa kuchangia maendeleo katika [nchi ya Kongo].”

Katika Novemba 17, 2000, Mashahidi wa Yehova walipewa Cheti cha Huduma Bora kwa sababu ya “kuchangia maendeleo ya raia wa Kongo [kupitia] elimu na mafundisho yaliyo katika vichapo vyao.”

Likitoa maelezo juu ya tuzo hilo, gazeti la Kinshasa Le Phare lilisema: “Ni vigumu kupata raia wa Kongo ambaye hajasoma gazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! au vichapo vinginevyo vinavyochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Magazeti hayo [huzungumzia] kila jambo linalohusu maisha.” Pia makala hiyo ilisema kwamba vichapo hivyo huonyesha “jinsi ya kukabiliana kwa mafanikio na matatizo ya sasa” na huonyesha “maana halisi ya matukio ya leo.” Kila toleo la Amkeni! “halijihusishi katika siasa na kutukuza jamii moja kuwa bora kuliko nyingine.” Isitoshe, vichapo hivyo husitawisha “uhakika katika ahadi ya Muumba ya dunia yenye amani na usalama ambayo hivi karibuni itachukua mahali pa huu mfumo mwovu wa sasa usiotii sheria.”

Kama ilivyotajwa na shirika la AJOCAD, vichapo vya Mashahidi wa Yehova vimenufaisha sana raia wengi wa Kongo. Ujumbe wao wenye tumaini ambao unapatikana katika lugha nyingi, unaweza kukunufaisha wewe pia.

Tafadhali soma habari iliyoonyeshwa hapa chini na uone jinsi inavyoweza kukunufaisha.