Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Andiko la Wakolosai 1:16 lasema kuhusu Mwana wa Mungu kwamba “vitu vingine vyote vimeumbwa kupitia yeye na kwa ajili yake.” Ni katika maana gani vitu vyote viliumbwa “kwa ajili ya” Mwana wa Mungu, Yesu?

Yehova alimtumia Mwana wake mzaliwa-pekee akiwa stadi wa kazi kuumba vitu vingine vyote, yaani, vitu vyote ila Yesu mwenyewe. (Mithali 8:27-30; Yohana 1:3) Kwa kufaa, Mwana hufurahia uumbaji huo, na ni katika maana hiyo uumbaji unakuwa “kwa ajili” yake.

Tunajua kwamba wazazi hutarajia kufurahishwa sana na watoto wao. Hivyo, mithali moja ya Biblia husema juu ya ‘mwana ambaye baba yake humfurahia.’ (Mithali 3:12, NW; 29:17) Vivyo hivyo, Yehova Mungu alifurahishwa na watu wake Israeli walipokuwa waaminifu. (Zaburi 44:3; 119:108; 147:11) Hata sasa, yeye pia hufurahishwa na uaminifu-mshikamanifu wa watu wake.—Mithali 12:22; Waebrania 10:38.

Hivyo, kwa kufaa Mungu angeacha Yesu, mfanyakazi mwenzake, afurahie kazi alizotimiza. Hata andiko la Mithali 8:31 lasema kwamba Mwana ‘alifurahia dunia inayokaliwa na watu; na furaha yake ilikuwa pamoja na wanadamu.’ Ni katika maana hiyo kwamba andiko la Wakolosai 1:16 lasema: “Vitu vingine vyote vimeumbwa kupitia yeye na kwa ajili yake.”