Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Tutaonana Katika Ufalme wa Mungu”

“Tutaonana Katika Ufalme wa Mungu”

“Tutaonana Katika Ufalme wa Mungu”

“Kwa Rafiki Mpendwa! Rupert, leo nimehukumiwa kifo. Usiomboleze kwa ajili yangu. Natuma salamu zangu kwako na kwa wote walio nyumbani. Tutaonana katika Ufalme wa Mungu.”

KATIKA Juni 8, 1942, Franc Drozg aliandika maneno hayo kabla hajapigwa risasi na askari wa Nazi. Kwa nini aliuawa?

Kulingana na rekodi katika Jumba la Makumbusho la Ukombozi wa Kitaifa huko Maribor, Slovenia, mfua chuma huyo mwenye umri wa miaka 38 alikataa kujiunga na kikosi cha jeshi la Ujerumani kilichokuwa kikimiliki nchi ya Slovenia. Alikuwa Bibelforscher, au Mwanafunzi wa Biblia, kama walivyoitwa Mashahidi wa Yehova katika eneo hilo. Kwa kufuata andiko la Isaya 2:4 alikataa kuunga mkono vita vya Wanazi, akisema kwamba yeye alikuwa raia wa Ufalme wa Mungu.—Mathayo 6:33.

Katika mji wa kwao wa Ptuj, Franc alijulikana kuwa mtangazaji mwenye bidii wa habari njema za Ufalme wa Mungu. (Mathayo 24:14) Licha ya magumu mengi, alihubiri habari njema bila kuacha hadi alipokamatwa mnamo Mei 1942.

Mashahidi wengi wa Yehova kutoka nchi ya Slovenia walinyanyaswa vikali na Wanazi. Franc alikuwa miongoni mwa Mashahidi wa kwanza kuuawa kwa sababu ya imani yake. Kama Wakristo wa karne ya kwanza, alitiwa moyo na maneno haya: “Lazima tuingie katika ufalme wa Mungu kupitia dhiki nyingi.” (Matendo 14:22) Alidhihirisha imani yake kwamba serikali ya kimbingu ni halisi kwa maneno haya yake ya mwisho, “Tutaonana katika Ufalme wa Mungu.”

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

Franc Drozg: Photo Archive-Museum of National Liberation Maribor, Slovenia; letter: Original kept in Museum of National Liberation Maribor, Slovenia