Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Henry wa Nane na Biblia

Henry wa Nane na Biblia

Henry wa Nane na Biblia

KATIKA kichapo chake History of the English-Speaking Peoples (Buku la 2), Winston Churchill aliandika hivi: “Kuhusiana na imani za kidini, yale Marekebisho Makubwa ya Kidini katika Ulaya yalileta badiliko kubwa. Biblia sasa ilipata kuwa na mamlaka mapya na makubwa zaidi. Kizazi cha zamani kiliyaona Maandiko Matakatifu kuwa hatari kwa watu wasio na elimu na kwamba yalipasa kusomwa tu na makasisi.”

Masimulizi hayo yanaendelea kusema: “Biblia nzima zilizochapwa, ambazo zilikuwa zimetafsiriwa kwa Kiingereza na Tyndal na Coverdale, zilikuwa zimetolewa kwa mara ya kwanza mwishoni mwa mwaka wa 1535, na sasa nakala kadhaa zilikuwa zikichapishwa. Serikali iliwashauri makasisi wawatie watu moyo waisome Biblia.” Kwa msaada wa serikali ya Henry wa Nane, wala si wa kanisa, Waingereza wangeweza kupata ujuzi wa Biblia ambao walikuwa wameukosa kwa karne nyingi. *

“Pigo jingine lilikipata kizazi hicho cha zamani wakati Serikali ilipoanzisha uchapaji wa Biblia nyingi za Kiingereza jijini Paris. Biblia hizo zilikuwa bora zaidi kuliko nakala zozote za hapo awali. Mnamo Septemba 1538, serikali hiyo iliagiza kila parokia nchini inunue Biblia kubwa ya Kiingereza na kuiweka katika kila kanisa, mahali ambapo wakazi wa parokia wangeweza kuisoma kwa urahisi. Nakala sita ziliwekwa katika kanisa kuu la Mtakatifu Paulo lililoko katika Jiji la London, na watu wengi sana walimiminika kwenye kanisa hilo mchana kutwa kuzisoma, hasa walipopata mtu yeyote mwenye sauti nzuri ambaye angeweza kusoma kwa sauti kubwa.”

Yasikitisha kwamba katika mataifa kadhaa, wengi hawatumii pendeleo walilo nalo la kuisoma Biblia kwa ukawaida. Jambo hilo linatia wasiwasi sana, kwa kuwa Biblia ndicho kitabu pekee ‘kilichopuliziwa na Mungu na ni chenye manufaa kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nidhamu katika uadilifu.’—2 Timotheo 3:16.

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 3 Mfalme Henry wa Nane alitawala Uingereza kuanzia mwaka wa 1509 hadi 1547.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

Henry wa Nane: Painting in the Royal Gallery at Kensington, from the book The History of Protestantism (Vol. I)