Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wafia-Imani wa Siku Hizi Watoa Ushahidi Nchini Sweden

Wafia-Imani wa Siku Hizi Watoa Ushahidi Nchini Sweden

Ripoti ya Watangazaji wa Ufalme

Wafia-Imani wa Siku Hizi Watoa Ushahidi Nchini Sweden

NENO la Kigiriki linalotafsiriwa “shahidi” ni martyr, na kutokana na neno hilo tunapata neno la Kiingereza “martyr,” linalomaanisha “mtu anayetoa ushahidi kupitia kifo.” Wakristo wengi wa karne ya kwanza walitoa ushahidi kuhusu Yehova kwa kufia imani yao.

Vivyo hivyo, katika karne ya 20 Mashahidi wengi sana waliuawa na vibaraka wa Hitler kwa kutounga mkono mambo ya kisiasa na ya kizalendo. Wafia-imani hao wa siku hizi pia wanatoa ushahidi wenye nguvu. Jambo hilo lilitokea nchini Sweden hivi majuzi.

Serikali ya Sweden ilianzisha kampeni kote nchini ya kuelimisha watu kuhusu yale Maangamizi Makubwa ili kuadhimisha miaka 50 tangu Vita ya Kwanza ya Ulimwengu iishe. Kampeni hiyo iliitwa Historia Iliyo Hai. Mashahidi wa Yehova walialikwa kushiriki na kueleza mambo yaliyowapata.

Mashahidi walikubali mwaliko huo na kutayarisha maonyesho waliyoyaita Wahasiriwa Waliosahaulika wa yale Maangamizi Makubwa. Maonyesho ya kwanza yalifanywa kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova huko Strängnäs. Mashahidi waliookoka yale Maangamizi Makubwa waliwaeleza wageni zaidi ya 8,400 waliohudhuria siku ya kwanza mambo yaliyowapata! Kufikia mwisho wa mwaka wa 1999, maonyesho hayo yalikuwa yameonyeshwa katika majumba ya makumbusho zaidi ya 100 na katika maktaba za umma kote nchini Sweden. Maonyesho hayo yalihudhuriwa na watu 150,000 hivi waliotia ndani maofisa kadhaa wa serikali ambao waliyasifu.

Hakuna tukio lolote linalohusiana na kazi ya Mashahidi wa Yehova nchini Sweden ambalo limewahi kutangazwa na kusifiwa sana jinsi hiyo. Wageni wengi waliuliza: “Mbona hamjatueleza mambo yaliyowapata wakati wa yale Maangamizi Makubwa?”

Baada ya maonyesho hayo kuonyeshwa katika eneo lao, kutaniko moja liliripoti kwamba mafunzo ya Biblia ya nyumbani yaliongezeka kwa asilimia 30! Shahidi mmoja alimwalika mfanyakazi mwenzake kwenye maonyesho hayo. Mfanyakazi huyo alikubali na akaja na rafikiye. Baadaye, rafiki huyo alisema kwamba hakuelewa jinsi ambavyo watu wangeweza kuwa na imani thabiti kiasi kwamba wangekuwa tayari kuuawa kuliko kutia sahihi hati ya kukana imani yao. Jambo hilo lilitokeza mazungumzo zaidi, na baadaye rafiki huyo akaanza kujifunza Biblia.

Kama wafia-imani wenzao wa karne ya kwanza, wafia-imani waaminifu wa karne ya 20 wametoa ushahidi kwa ujasiri kwamba tunastahili kuwa na imani thabiti na kuwa waaminifu-washikamanifu kwa Yehova, Mungu wa pekee wa kweli.—Ufunuo 4:11.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 13]

Mfungwa wa kambi: Państwowe Muzeum Oświęcim-Brzezinka, courtesy of the USHMM Photo Archives