Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Tukio Muhimu Zaidi Katika Historia

Tukio Muhimu Zaidi Katika Historia

Tukio Muhimu Zaidi Katika Historia

TUKIO hilo lilikuwa kifo cha Yesu. Kwa nini kifo chake ni muhimu sana? Kwa sababu kadhaa.

Uaminifu wa Yesu hadi kifo ulithibitisha kwamba mwanadamu anaweza kudumisha uaminifu-maadili kwa Mungu.

Kifo cha Yesu kiliwaandalia wanadamu wengine fursa ya kuja kutawala pamoja naye mbinguni. Pia kiliwafungulia wengine wengi njia ya kuja kufurahia uhai wa milele katika dunia paradiso.

Usiku uliotangulia kifo chake, Yesu alitumia divai nyekundu na mkate usiotiwa chachu kama mifano ya dhabihu yake yenye upendo ya kibinadamu. Aliwaambia wafuasi wake hivi: “Fulizeni kufanya hili katika ukumbuko wangu.” (Luka 22:19) Je, wewe utakumbuka tukio hilo muhimu?

Mashahidi wa Yehova wanakualika kwa uchangamfu ujiunge nao katika kuadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Yesu. Tarehe ya mwadhimisho huo mwaka huu itakuwa Alhamisi, Machi 28, baada ya jua kutua. Unaweza kuhudhuria mwadhimisho huo katika Jumba la Ufalme lililo karibu nawe. Tafadhali pata habari kutoka kwa Mashahidi wa Yehova walio karibu nawe kuhusu saa na mahali barabara.