Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wakati Inapokuwa Jambo la Hekima Kutoroka

Wakati Inapokuwa Jambo la Hekima Kutoroka

Wakati Inapokuwa Jambo la Hekima Kutoroka

ULIMWENGU wa leo umejaa ujasiri wa kujionyesha tu, uhasama, na vishawishi. Mtu anayetoroka hali fulani huonwa kuwa dhaifu au mwoga. Huenda hata akadhihakiwa.

Hata hivyo, Biblia huonyesha waziwazi kwamba nyakati nyingine ni jambo la hekima na la ujasiri kutoroka. Akithibitisha ukweli huo, Yesu Kristo aliwaambia hivi wanafunzi wake kabla ya kuwatuma kwenda katika huduma: “Wakati wawanyanyasapo nyinyi katika jiji moja, kimbilieni jingine.” (Mathayo 10:23) Naam, wanafunzi wa Yesu walipaswa kujaribu kuwatoroka wanyanyasi wao. Hawakupaswa kupigana vita vya kidini na kujaribu kugeuza watu imani kwa nguvu. Walikuwa na ujumbe wa amani. (Mathayo 10:11-14; Matendo 10:34-37) Kwa hiyo, badala ya kukasirika, Wakristo walipaswa kutoroka kutoka mahali palipo na ugomvi. Kwa kufanya hivyo, wangedumisha dhamiri safi na vilevile uhusiano wao wenye thamani pamoja na Yehova.—2 Wakorintho 4:1, 2.

Mfano ulio tofauti na huo wapatikana katika kitabu cha Biblia cha Mithali. Kinasimulia kuhusu mwanamume kijana ambaye badala ya kutoroka alipokabili kishawishi, alimfuata kahaba, “kama vile ng’ombe aendavyo machinjoni.” Matokeo yakawaje? Alipatwa na msiba kwa sababu ya kushindwa na kishawishi kilichohatarisha uhai wake.—Mithali 7:5-8, 21-23.

Utafanyaje ukikabili kishawishi cha kufanya uasherati au ukikabili hali nyingine hatari? Kulingana na Neno la Mungu, hatua inayofaa ingekuwa kutoka mahali hapo mara moja.—Mithali 4:14, 15; 1 Wakorintho 6:18; 2 Timotheo 2:22.