Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Tetragramatoni Katika Tafsiri ya Septuagint

Tetragramatoni Katika Tafsiri ya Septuagint

Tetragramatoni Katika Tafsiri ya Septuagint

JINA la Mungu, Yehova, linawakilishwa na Tetragramatoni, yaani, herufi nne za Kiebrania יהוה (YHWH). Kwa muda mrefu iliaminiwa kwamba herufi hizo hazikutumiwa katika tafsiri za Septuagint. Hivyo, ilisemekana kwamba waandishi wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo hawakutumia jina la Mungu katika maandishi yao waliponukuu Maandiko ya Kiebrania.

Uvumbuzi mbalimbali uliofanywa katika miaka mia moja hivi iliyopita ulionyesha kwamba jina la Mungu lilitumiwa katika tafsiri ya Septuagint. Kichapo kimoja kinasema: “Wayahudi wa Ugiriki walitaka sana kulihifadhi jina hilo takatifu la Mungu hivi kwamba walipotafsiri Biblia ya Kiebrania katika Kigiriki, walinakili herufi hizo za Tetragramatoni katikati ya maandishi ya Kigiriki.”

Kipande kinachoonyeshwa upande wa kushoto ni mfano mmoja tu wa mafunjo kadhaa yenye maandishi hayo ambayo yamesalia. Kipande hicho cha tangu karne ya kwanza W.K., kimepewa namba 3522 na kinapatikana huko Oxyrhynchus, Misri. * Kina ukubwa wa sentimeta 7 kwa 10.5 hivi na maandishi yake ni kutoka Ayubu 42:11, 12. Tetragramatoni, ambazo zimezungushiwa duara, zinapatikana katika herufi za zamani za Kiebrania. *

Kwa hiyo, je, jina la Mungu lilitumiwa katika nakala za mapema za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo? Msomi George Howard anasema hivi: “Kwa kuwa Tetragramu zilikuwa bado zinatumiwa katika nakala za Biblia ya Kigiriki [Septuagint] iliyotumiwa katika kanisa la mapema, ni jambo la akili kuamini kwamba waandishi wa A[gano] J[ipya] walihifadhi herufi Tetragramu katika maandishi ya Biblia waliponukuu Maandiko.” Inaonekana kwamba baadaye, wanakili walitumia maneno Kyʹri·os (Bwana) na The·osʹ (Mungu) badala ya jina la Mungu.

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 4 Ili kupata habari zaidi kuhusu mafunjo yanayopatikana huko Oxyrhynchus, ona gazeti la Mnara wa Mlinzi la Februari 15, 1992, ukurasa wa 26-28.

^ fu. 4 Ili kupata mifano mingine ya jina la Mungu katika tafsiri za zamani za Kigiriki, ona New World Translation of the Holy Scriptures−With References, nyongeza 1C.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 30]

Courtesy of the Egypt Exploration Society