Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wakati wa Kufunua Siri

Wakati wa Kufunua Siri

Wakati wa Kufunua Siri

Kutunza siri kunaweza kuzuia migogoro na kudumisha amani. Lakini je, kuna wakati wa kufunua siri? Ona anayosema nabii Amosi kuhusu Mungu wake: “MUNGU hatafanya neno lolote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.” (Amosi 3:7) Kutokana na maneno hayo tunaweza kujifunza jambo fulani kuhusu kutunza siri. Yehova anaweza kuweka habari fulani kuwa siri kwa muda fulani na hatimaye kuifunua kwa watu fulani. Tunaweza kumwigaje Yehova kuhusiana na jambo hilo?

Nyakati fulani, wachungaji waliowekwa rasmi katika kutaniko la Kikristo huona kwamba inafaa kutofunua habari fulani. (Matendo 20:28) Kwa mfano, kwa kufikiria hali ya kutaniko, huenda wakaamua kutofunua habari zinazohusu mipango fulani au mabadiliko yanayohusu madaraka kutanikoni, hadi wakati hususa.

Hata hivyo, katika hali hiyo, inafaa kuwajulisha wote wanaohusika iwapo habari hiyo itafunuliwa, na ni wakati gani itakapofunuliwa. Kujua ni wakati gani habari fulani itakapofunuliwa kunaweza kuwasaidia kutunza siri hiyo.—Mithali 25:9.