Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

‘Mungu, Kwa Nini Uliruhusu Msiba Huu Utokee?’

‘Mungu, Kwa Nini Uliruhusu Msiba Huu Utokee?’

‘Mungu, Kwa Nini Uliruhusu Msiba Huu Utokee?’

RICARDO bado anakumbuka wakati alipoketi na mke wake Maria katika chumba cha wanaosubiri daktari. * Wote wawili hawakuwa na ujasiri wa kusoma matokeo ya uchunguzi wa kitiba ambao Maria alikuwa amefanyiwa karibuni. Baadaye, Ricardo alifungua bahasha iliyokuwa na ripoti ya daktari na wote wakaipitia haraka-haraka. Waliona neno “kansa,” kisha wakaanza kulia kwa kuwa walielewa kabisa kilichomaanishwa na neno hilo.

Ricardo anasema hivi: “Daktari alikuwa mwenye fadhili sana, lakini yaonekana alielewa hiyo ilikuwa hali ngumu kwa sababu alituambia tena na tena kwamba tunapaswa kumtumaini Mungu.”

Kabla ya Maria kuanza kutibiwa kwa kutumia mionzi, daktari wake aliona kwamba mguu wake wa kulia ulikuwa unatetemeka. Alipopimwa tena, iligunduliwa kwamba kansa hiyo ilikuwa imesambaa hadi kwenye ubongo wake. Baada ya juma moja tu, matibabu hayo ya mionzi yalisimamishwa. Maria alipoteza fahamu na akafa miezi miwili baadaye. “Nilifurahi kwamba mateso yake yalikoma,” aeleza Ricardo, “lakini nilimkosa sana hivi kwamba nilianza kutamani kufa pia. Mara kwa mara nilimlilia Mungu: ‘Kwa nini uliruhusu msiba huu utokee?’”

Watu Huuliza Maswali Mengi Wanapopatwa na Msiba

Kama Ricardo, watu wengi duniani hulazimika kukabiliana na hali ya kuteseka. Mara nyingi watu wasio na hatia ndio huteseka. Fikiria huzuni kubwa inayosababishwa na vita vya wanadamu visivyokoma. Au fikiria maumivu wanayopata watu ambao walibakwa, wakatendewa vibaya wakiwa watoto, wakatendewa kikatili nyumbani, na mambo mengine maovu. Inaonekana kwamba katika historia yote wanadamu wameendelea kutendeana mambo yasiyo ya haki na yenye kuumiza. (Mhubiri 4:1-3) Kuna wengine ambao wamekumbwa na misiba ya asili au magonjwa ya kihisia-moyo, kiakili, na kimwili. Si ajabu kwamba wengi huuliza, “Kwa nini Mungu huruhusu mateso hayo?”

Si rahisi hata kwa wale walio na imani kukabiliana na kuteseka. Huenda hata wewe ukashangaa ni kwa sababu gani Mungu mwenye upendo na nguvu zote huruhusu wanadamu wateseke. Kupata jibu lenye kuridhisha na la kweli kwa swali hilo lenye kutatanisha ni muhimu ili tudumishe amani ya akili na uhusiano wetu pamoja na Mungu. Biblia hujibu swali hilo. Tafadhali chunguza vile inavyosema katika makala ifuatayo.

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 2 Majina yamebadilishwa.

[Picha katika ukurasa wa 3]

Daktari alituambia tena na tena kwamba tunapaswa kumtumaini Mungu