Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Umaskini Utakwisha?

Je, Umaskini Utakwisha?

Je, Umaskini Utakwisha?

“TAZAMA, machozi yao waliodhulumiwa, ambao walikuwa hawana mfariji; na upande wa wale waliowadhulumu kulikuwa na uwezo, walakini wale walikuwa hawana mfariji,” akasema Mfalme Sulemani wa Israeli la kale. (Mhubiri 4:1) Bila shaka, wengi wa watu waliodhulumiwa ambao Sulemani anataja walikuwa maskini.

Kiwango cha umaskini hakiwezi kukadi- riwa kwa kutegemea tu mapato ya watu. Kulingana na takwimu za Benki ya Dunia za Juni 2002, “imekadiriwa kwamba mnamo mwaka wa 1998, watu bilioni 1.2 ulimwenguni pote waliishi kwa mapato yanayopungua dola 1 kwa siku . . . nao wengine bilioni 2.8 kwa mapato yanayopungua dola 2 kwa siku.” Ripoti hiyo ilisema kwamba ingawa idadi hiyo ilikuwa imepungua ikilinganishwa na makadirio ya awali, “bado takwimu hizo ziko juu na zinaonyesha kwamba watu wengi ni maskini.”

Je, umaskini utakwisha? Yesu Kristo aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Mna maskini pamoja nanyi sikuzote.” (Yohana 12:8) Je, hiyo inamaanisha kwamba umaskini na madhara yake yataendelea milele? La, ijapokuwa Yesu hakuahidi wafuasi wake kwamba wote wangekuwa matajiri, hatuwezi kukata kauli kwamba maskini hawana tumaini.

Ijapokuwa mara kwa mara jitihada na aha- di za wanadamu za kumaliza umaskini zimeambulia patupu, Neno la Mungu, Biblia, linatuhakikishia kwamba karibuni hakutakuwa na watu maskini. Kwa kweli, Yesu alitangaza “habari njema kwa walio maskini.” (Luka 4:18) Habari njema hizo zinatia ndani ahadi ya kwamba umaskini utakomeshwa. Ahadi hiyo itatimizwa wakati Ufalme wa Mungu utaleta hali zenye uadilifu duniani.

Dunia itakuwa tofauti kama nini wakati huo! Mfalme wa mbinguni Yesu Kristo “atamhurumia aliye dhaifu na maskini, na nafsi za wahitaji ataziokoa.” Kwa kweli, “atawakomboa nafsi zao na kuonewa na udhalimu.”—Zaburi 72:13, 14.

Kuhusu wakati huo, andiko la Mika 4:4 linasema: “Wataketi kila mtu chini ya mzabibu wake, na chini ya mtini wake; wala hapana mtu atakayewatia hofu; kwa kuwa kinywa cha BWANA wa majeshi kimesema hivi.” Ufalme wa Mungu utatatua matatizo yote ya wanadamu, hata kukomesha magonjwa na kifo. Mungu ‘atameza mauti hata milele; na Bwana MUNGU atafuta machozi katika nyuso zote.’—Isaya 25:8.

Unaweza kutumaini ahadi hizo kwa sababu zimeandikwa kwa roho ya Mungu mwenyewe. Mbona usichunguze uthibitisho unaoonyesha kwamba unabii wa Biblia unategemeka?

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

FAO photo/M. Marzot