Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Unakaribishwa kwa Uchangamfu

Unakaribishwa kwa Uchangamfu

Unakaribishwa kwa Uchangamfu

MLO wa Jioni wa Bwana ambao Bwana Yesu Kristo alianzisha miaka ipatayo 2,000 iliyopita, si tukio tu la kihistoria. Mlo huo umekuwa na matokeo makubwa kwa watu tangu uanzishwe. Kwa kuchochewa na yale wanayosoma katika vitabu vya Injili kuhusu yaliyotokea usiku huo, wengi wamejitahidi kuadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana kwa njia mbalimbali.

Wengi wanafanya hivyo kwa sababu Yesu Kristo mwenyewe aliwaamuru wafuasi wake waadhimishe tukio hilo na wafanye hivyo kwa ukawaida. Aliwaambia hivi kinaganaga: “Fulizeni kufanya hili katika ukumbuko wangu.”—Luka 22:19; 1 Wakorintho 11:23-25.

Bila shaka, ili mwadhimisho huo uwe wenye kuthawabisha kikweli, mtu anapaswa kufahamu maana yake kama inavyoelezwa katika Neno la Mungu Biblia. Zaidi ya hayo, ni muhimu kujua yale ambayo Biblia husema kuhusu wakati na jinsi tukio hilo linavyopaswa kuadhimishwa.

Kwa kutii amri ya Yesu, Mashahidi wa Yehova ulimwenguni kote watakusanyika pamoja Jumatano jioni, Aprili 16, 2003, ili kuadhimisha kifo cha Yesu. Hiyo itakuwa pindi ya kuchunguza Maandiko na kuimarisha imani yao na upendo wao kwa Yesu Kristo, aliyesema: “Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akatoa Mwana mzaliwa-pekee wake, ili kila mtu anayedhihirisha imani katika yeye asipate kuangamizwa bali awe na uhai udumuo milele.” (Yohana 3:16) Unakaribishwa kwa uchangamfu kukusanyika pamoja nao jioni hiyo ili wewe pia uweze kuimarisha imani yako na upendo wako kwa Yesu Kristo na Baba wa mbinguni Yehova Mungu.