Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Wakumbuka?

Je, Wakumbuka?

Je, Wakumbuka?

Je, umefurahia kusoma matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona kama unaweza kujibu maswali yafuatayo:

Tunawezaje kunufaika kwa kujifunza kuhusu familia ya Shafani?

Shafani alikuwa mnakili na mwandishi wa Mfalme Yosia wa Yuda. Shafani alikuwa mtu mashuhuri katika ufalme huo, naye aliunga mkono kampeni ya mfalme ya kurudisha ibada ya kweli. Wana wawili wa Shafani walikuwa waaminifu kwa nabii Yeremia. Vivyo hivyo, mwana mwingine na wajukuu wawili walitumia mamlaka yao kutetea ibada ya kweli. Sisi pia tunapaswa kutumia mali na mamlaka yetu ili kutetea ibada ya kweli.—12/15, ukurasa wa 19-22.

Irene Hochstenbach aliwezaje kumtumikia Yehova ijapokuwa yeye ni kiziwi?

Alipokuwa na umri wa miaka saba alipoteza uwezo wake wa kusikia. Ijapokuwa yeye ni kiziwi, amejifunza kuwasiliana na wengine na sasa anaambatana na mume wake (mwangalizi wa mzunguko) anapotembelea makutaniko huko Uholanzi.—1/1, ukurasa wa 23-26.

Ni vitabu gani viwili vilivyotolewa kwenye Makusanyiko ya Wilaya ya “Watangazaji wa Ufalme Wenye Bidii”?

Wakristo ulimwenguni pote walifurahi kupokea kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli, ambacho kimekusudiwa kutumiwa katika funzo pamoja na wapya baada ya kumaliza kujifunza kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele; kitabu kingine kipya ni Mkaribie Yehova, kinachokazia sifa na matendo ya Yehova. Pia kitabu hicho kinaonyesha jinsi tunavyoweza kuiga sifa zake.—1/15, ukurasa wa 23, 24.

Andiko la Mithali 12:5, linalosema, “Mawazo ya mwenye haki ni adili,” linamaanisha nini?

Mawazo ya watu wema ni ya uadilifu nayo huwaongoza kutenda kwa njia ya haki bila ubaguzi. Nia ya wenye haki ni njema kwa kuwa wao huchochewa na upendo wao kwa Mungu na wanadamu wenzao.—1/15, ukurasa wa 30.

Ni nini kinachoweza kumsaidia mtu kusitawisha maoni yanayofaa kuhusu kazi?

Ni vizuri kuzoezwa kuthamini kazi tangu utotoni. Biblia inatutia moyo tuwe na maoni yanayofaa kuhusu kazi na kuepuka uvivu. (Mithali 20:4) Pia inawatia moyo Wakristo wasifanye kazi kupita kiasi. Tunapaswa kutambua kwamba utumishi kwa Mungu unapaswa kuwa muhimu maishani mwetu. (1 Wakorintho 7:29-31) Isitoshe, Wakristo wa kweli wana hakika kwamba Mungu hatawaacha.—2/1, ukurasa wa 4-6.

Ni wapi katika Biblia ambapo madhabahu inatajwa kwa mara ya kwanza?

Ni katika andiko la Mwanzo 8:20, linalotaja madhabahu iliyojengwa na Nuhu alipotoka katika safina baada ya Gharika. Hata hivyo, inaelekea kwamba Kaini na Abeli walitumia madhabahu walipotoa dhabihu zao. (Mwanzo 4:3, 4)—2/15, ukurasa wa 28.

Wakristo fulani wanawezaje kutumia kwa hekima hali zenye kubadilika maishani?

Baadhi yao wamekubali mabadiliko, au kufanya mabadiliko kazini ili wapate wakati zaidi kwa ajili ya huduma. Wengine wameweza kuongeza utumishi wao kwa Mungu wakati madaraka ya familia yanapopungua, kwa mfano, wakati watoto wao wanapokuwa watu wazima na kufunga ndoa.—3/1, ukurasa wa 19-22.

Mfano wa Yona na mtume Petro unatusaidiaje kuwaona wengine kama Yehova anavyowaona?

Yona na Petro walifanya makosa yanayojulikana sana kuhusiana na kufikiri kwao, na namna walivyotenda, imani na utii wao ulipojaribiwa. Hata hivyo, ni wazi kwamba Yehova alitambua sifa zao nzuri na aliendelea kuwatumia katika utumishi wake. Wengine wanapotuudhi au kutuvunja moyo, tunaweza kufikiria sifa zao nzuri zilizotuvutia zamani na sifa zao nzuri ambazo Mungu huona.—3/15, ukurasa wa 16-19.

Kwa nini sura na mistari ya kitabu cha Zaburi hutofautiana katika tafsiri mbalimbali za Biblia?

Sura na mistari ya kitabu hicho katika lugha ya awali ya Kiebrania hutofautiana na tafsiri ya Kigiriki ya Septuagint. Tafsiri nyingi za karibuni, huenda zikatofautiana, ikitegemea kama zimetafsiriwa kutoka kwa maandishi ya Kiebrania au tafsiri ya Septuagint.—4/1, ukurasa wa 31.