Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Chagua Uhai wa Milele

Chagua Uhai wa Milele

Chagua Uhai wa Milele

SIKU hizi kuna mambo mengi ambayo watu wanaweza kuchagua kufanya kuliko wakati mwingine wowote. Kwa mfano, mara nyingi sisi huchagua mavazi tutakayovaa, chakula tutakachokula, mahali tutakapofanya kazi, na pia tutakapoishi. Katika sehemu nyingi ulimwenguni ni kawaida pia mtu kujichagulia mwenzi wa ndoa. Hata hivyo, Biblia inaonyesha kwamba kuna jambo fulani bora zaidi ambalo wanadamu wote wanaweza kuchagua.

Biblia inasema: “Haki huelekea uzima; afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe.” (Mithali 11:19) Naye Yesu Kristo alisema: ‘Hii yamaanisha uhai udumuo milele, wao kuendelea kutwaa ujuzi juu yako wewe, Mungu pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.’—Yohana 17:3.

Naam, Muumba wetu ametupatia fursa ya kuchagua njia inayoongoza kwenye uhai wa milele! Tunapaswa kufanya nini ili tuupate?

Biblia inasema, “katika njia ya haki kuna uhai.” (Mithali 12:28) Tunaweza kuwa miongoni mwa wenye haki walio katika njia inayoongoza kwenye uhai wa milele. Jinsi gani? Kwa kuhakikisha kwamba tunaishi kupatana na mapenzi na amri za Mungu. (Mathayo 7:13, 14) Kwa hiyo, na tufanye uchaguzi unaofaa na kupokea zawadi ya uhai wa milele kutoka kwa Mungu.—Waroma 6:23.