Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Ni Desturi Tu au Ni Hongo?

Je, Ni Desturi Tu au Ni Hongo?

Je, Ni Desturi Tu au Ni Hongo?

KATIKA vyuo fulani nchini Poland, wanafunzi wana desturi ya kukusanya pesa za kuwanunulia walimu wao zawadi ili wapate alama za juu katika mitihani yao. Kwa hiyo haishangazi kwamba Mkristo mchanga anayeitwa Katarzyna alikabili hali ngumu. Alijiuliza, “je, nitoe pesa au nisitoe?” Wanafunzi wenzake walimwambia: “Hiyo ni desturi ya kawaida. Hutapata hasara yoyote, bali utaweza kufaidika, mbona una shaka?”

Katarzyna anakiri hivi: “Katika mwaka wangu wa kwanza chuoni, nilishiriki kukusanya pesa. Lakini baadaye nilitambua kwamba kwa kufanya hivyo nilikuwa nikiunga mkono hongo ambayo imekataliwa katika Biblia.” Alikumbuka maandiko yanayoonyesha kwamba Yehova anachukia hongo kabisa. (Kumbukumbu la Torati 10:17; 16:19; 2 Mambo ya Nyakati 19:7) Katarzyna anasema: “Nilielewa jinsi ilivyo rahisi kushindwa na msongo kutoka kwa wanafunzi wenzako. Nilifikiria sana jambo hilo na tangu wakati huo sijashiriki tena desturi hiyo.” Ingawa amekuwa akidhihakiwa na wanafunzi wengine, kwa muda wa miaka mitatu, aliweza kuwaeleza baadhi yao kwamba hashiriki kukusanya pesa za kununua “zawadi” kwa sababu ya imani yake inayotegemea Biblia.

Baadhi yao walimlaumu Katarzyna kuwa mchoyo na asiyewajali wengine. Yeye anasema hivi: “Bado sipatani kabisa na wengine. Lakini wengi wanaheshimu maoni yangu, na hilo hunifurahisha.” Katarzyna alijulikana kama Shahidi wa Yehova anayetii kanuni za Biblia maishani mwake.