Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Faraja kwa Wanaolilia Msaada

Faraja kwa Wanaolilia Msaada

Faraja kwa Wanaolilia Msaada

BIBLIA si kitabu kinachozungumzia afya ya akili. Hata hivyo, Biblia hutufariji na kutusaidia kuthamini uhai ijapokuwa tunapatwa na matatizo. Kwa kufaa, Maandiko yanasema: “Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu.” (Ayubu 14:1) Baadhi ya majaribu yetu husababishwa na hali yetu ya kutokamilika. Lakini ni nani hasa husababisha kuteseka kwa wanadamu?

Biblia inamtaja huyo kuwa roho mwovu, anayeitwa Ibilisi na Shetani. Yeye ‘anaiongoza vibaya dunia nzima inayokaliwa’ naye husababisha mengi ya matatizo yanayowapata wanadamu. Hata hivyo, Biblia pia inatuambia kwamba wakati wake unakaribia kwisha. (Ufunuo 12:9, 12) Hivi karibuni, Mungu atayamaliza mateso yote ambayo Shetani amewasababishia wakaaji wa dunia. Biblia inasema kwamba ulimwengu mpya ambao Mungu ameahidi utakomesha hali ya kukata tamaa.—2 Petro 3:13.

Inafariji kama nini kujua kwamba kuteseka kwa wanadamu ni kwa muda tu! Chini ya Ufalme wa mbinguni wa Mungu mikononi mwa Yesu Kristo, ukosefu wa haki na kuteseka kutakoma. Kuhusu Mfalme aliyewekwa na Mungu, Maandiko yanasema: “Atamkomboa mhitaji aliapo [“maskini anayelilia msaada,” NW], na mtu aliyeonewa iwapo hana msaidizi. Atamhurumia aliye dhaifu na maskini, na nafsi za wahitaji ataziokoa. Atawakomboa nafsi zao na kuonewa na udhalimu, na damu yao ina thamani machoni pake.”—Zaburi 72:12-14.

Wakati wa kutimizwa kwa unabii huo unakaribia sana. Tunaweza kufurahia uhai wa milele katika dunia paradiso chini ya hali bora sana. (Luka 23:43; Yohana 17:3) Kujua ahadi hizo za Biblia huwafariji na kuwapa tumaini watu wanaolilia msaada.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

Depressed girl: Photo ILO/J. Maillard