Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unasitawisha Hisia ya Kustaajabu?

Je, Unasitawisha Hisia ya Kustaajabu?

Je, Unasitawisha Hisia ya Kustaajabu?

JE, UMEONA kwamba waandikaji wa Biblia huchochea hisia ya kustaajabu wanapotaja kazi na sifa za Mungu? “Nimeumbwa kwa njia ya ajabu,” akasema mtunga-zaburi. (Zaburi 139:14) Nabii Isaya aliandika: “Ee Yehova, wewe ni Mungu wangu. Ninakutukuza, ninalisifu jina lako, kwa maana umetenda mambo ya ajabu.” (Isaya 25:1) Au fikiria hali ya kustaajabu inayoonyeshwa na maneno haya ya mtume Paulo: “Lo! Jinsi kilivyo kina cha utajiri wa Mungu na hekima!”—Waroma 11:33.

Kamusi ya Kiswahili Sanifu inafafanua neno “staajabu” kuwa “mshtuko wa mwili au mawazo kwa kuona, kusikia au kuhisi kitu au jambo ambalo si la kawaida au ambalo halikutarajiwa.”

Inafurahisha kuwaona watoto wadogo wakistaajabu wanapoona, kuhisi, au kusikia mambo mapya. Inasikitisha kwamba mara nyingi mtoto anapokomaa, hastaajabu sana anapoona mambo mapya.

Hata hivyo, kwa waandishi wa Biblia waliotajwa juu, kustaajabu kulikuwa sehemu ya utu wao. Hisia hiyo ilikuwa ya kudumu. Kwa nini? Walisitawisha hisia ya kustaajabu kwa kutafakari kwa uthamini kazi za Mungu. Mtunga-zaburi alisali: “Nimezikumbuka siku za kale, nimeyatafakari matendo yako yote, naziwaza kazi za mikono yako.”—Zaburi 143:5, Union Version.

Inapendeza kuona kwamba leo waabudu wa Mungu wana hisia hiyo ya kustaajabu! Je, wewe unayo? Je, unaisitawisha?