Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Mungu Anatujali?

Je, Mungu Anatujali?

Je, Mungu Anatujali?

E, WEWE hujikuta umelemewa na hisia kwa sababu ya matatizo ya familia, afya, kazi, au madaraka mengine mazito? Watu wengi hujikuta katika hali hiyo. Leo, hakuna mtu asiyeathiriwa na ukosefu wa haki, uhalifu, na jeuri. Naam, hali leo inafanana kabisa na vile Biblia isemavyo: “Uumbaji wote unaendelea kuugua pamoja na kuwa katika maumivu pamoja mpaka sasa.” (Waroma 8:22) Si ajabu kwamba watu wengi huuliza hivi: ‘Je, Mungu anajali? Je, atatusaidia?’

Mfalme Sulemani mwenye hekima alimwambia Mungu hivi katika sala: ‘Wewe peke yako unajua vema moyo wa wanadamu.’ Sulemani aliamini kwamba Mungu anatujua na pia anatujali tukiwa mtu mmoja-mmoja. Alimwomba Mungu ‘asikie akiwa mbinguni’ na kujibu sala za kila mtu mwenye kumwogopa na anayemweleza “pigo lake na maumivu yake mwenyewe.”—2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30.

Leo, Yehova Mungu bado anatujali naye hutualika tusali kwake. (Zaburi 50:15) Yeye anaahidi kwamba atajibu sala za kutoka moyoni zinazopatana na mapenzi yake. (Zaburi 55:16, 22; Luka 11:5-13; 2 Wakorintho 4:7) Naam, Yehova husikiliza “sala yoyote, ombi lolote la kutaka kibali ambalo huenda likatolewa na mwanadamu au na watu [wake].” Kwa hiyo, Mungu atatutunza na kutuongoza kwa upendo ikiwa tutamtumaini, kumwomba msaada, na kumkaribia. (Mithali 3:5, 6) Mwandikaji wa Biblia Yakobo anatuhakikishia hivi: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.”—Yakobo 4:8.