Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Huendelea Kukutembelea?

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Huendelea Kukutembelea?

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Huendelea Kukutembelea?

Huduma ya nyumba kwa nyumba ambayo Mashahidi wa Yehova hufanya kwa bidii inajulikana sana duniani kote. Wengine hujiuliza kwa nini Mashahidi huendelea kuwatembelea, hasa ikiwa hapo awali hawakupendezwa sana na ujumbe wao. Barua mbili kutoka Urusi zinaeleza sababu.

“Kusema kweli,” anakiri Masha, msichana mwenye umri wa miaka 19 anayeishi Khabarovsk, “hapo zamani, niliwaepuka Mashahidi wa Yehova kabisa.” Hata hivyo, baada ya kusoma nakala chache za magazeti yanayochapishwa na Mashahidi, alibadili mtazamo wake. Masha anaandika: “Mambo niliyosoma yalikuwa yenye kupendeza na yenye kuelimisha sana, lakini jambo lililo muhimu zaidi ni kwamba yanakufanya uwe na maoni tofauti kuhusu ulimwengu. Pole kwa pole nilianza kuelewa kusudi la maisha.”

Svetlana, anayeishi katika jiji la Ussuriysk, lililo kilometa 80 kaskazini ya Vladivostok, anaandika hivi: “Nimeanza kusoma Mnara wa Mlinzi na Amkeni! hivi karibuni. Magazeti hayo yanahitajiwa sana wakati huu. Ninafurahia makala zote. Ni yenye kupendeza, kuarifu, na kuelimisha. Asanteni! Asanteni sana kwa sababu ya ninyi kuwa katika ulimwengu huu na kwa kufanya kazi hiyo ya fadhili na muhimu.”

Mashahidi wa Yehova duniani kote huchukua kwa uzito swali hili la mtume Paulo lenye kuamsha fikira: “Nao [watu] watasikiaje bila mtu wa kuhubiri?” (Waroma 10:14) Kwa nini usiwasikilize Mashahidi kwa dakika chache watakapokutembelea tena? Wewe pia unaweza kufurahia ujumbe wa faraja unaopatikana katika Neno la Mungu, Biblia.