Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Imani Inaweza Kumponya Mgonjwa?

Je, Imani Inaweza Kumponya Mgonjwa?

Je, Imani Inaweza Kumponya Mgonjwa?

TUNAPOKUWA wagonjwa, sisi hutafuta kitulizo na ponyo. Yaelekea umesoma katika Biblia kwamba mara nyingi Yesu Kristo aliponya aina zote za magonjwa, jambo lililowaletea wagonjwa wengi kitulizo. Aliwaponyaje? Kwa ‘nguvu za Mungu,’ Biblia inasema. (Luka 9:42, 43; Matendo 19:11, 12) Hivyo, roho takatifu ya Mungu ndiyo iliyofanya mgonjwa apone wala si imani yake tu. (Matendo 28:7-9) Hiyo ndiyo sababu Yesu hakuwataka wagonjwa wamwamini ili awaponye.

Huenda ukajiuliza: ‘Je, kuponya kimuujiza kumetoweka, au je, maponyo kama yale aliyofanya Yesu yatatokea tena? Kuna tumaini gani kwa wale wanaougua ugonjwa wenye maumivu usioweza kupona?’

Biblia inaeleza kwamba katika ulimwengu mpya wa Mungu wenye uadilifu, nguvu za Mungu zitafanya kuwepo tena na maponyo ya kimuujiza kama yale yaliyofanywa na Yesu alipokuwa duniani. Mashahidi wa Yehova katika mahali unapoishi watafurahi kukuonyesha ni wakati gani na jinsi gani Mungu atatimiza yale ambayo wale wanaoponya kwa imani hawawezi kutimiza, yaani, kuondoa magonjwa yote, na pia kifo. Naam, Mungu “atameza kifo milele.”—Isaya 25:8.