Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Biblia Ilimsaidia Kushinda Kishawishi

Biblia Ilimsaidia Kushinda Kishawishi

Biblia Ilimsaidia Kushinda Kishawishi

Leo kuna vishawishi vingi ulimwenguni. Si rahisi kufuata viwango vya Biblia. Kwa mfano, huenda ikawa vigumu kufuata shauri hili la Biblia: “Ukimbieni uasherati.”—1 Wakorintho 6:18.

Shahidi mmoja wa Yehova ambaye tutamwita Sebastian, alikuwa akifanya kazi katika kampuni fulani ya nchi za Skandinavia huko Poland. Alihitaji kujitahidi sana ili kudumisha utimilifu wake.

Wafanyakazi wenzake walimjua Sebastian kuwa Shahidi wa Yehova. Wakubwa wake kazini, walimpa mapendeleo mengi kwa sababu walithamini bidii na mwenendo wake mzuri. Hata hivyo, alitambua kwamba mapendeleo hayo yalihusisha mikutano ya biashara ambayo ingekuwa na vitumbuizo visivyofaa.

Muda si muda, Sebastian alianza kuwa na shaka. “Mkubwa wangu wa kazi anajua kwamba mimi ni Shahidi wa Yehova. Hiyo ndiyo sababu ananiamini na kunitegemea. Nikikataa kuhudhuria mikutano hiyo, nitapoteza kazi, ambayo ilikuwa vigumu kuipata. Namna gani nikihudhuria kama mtazamaji tu?”

Halafu, Sebastian akapata habari zaidi kuhusu mambo aliyotarajiwa kufanya. Angetarajiwa “kuwatunza” wateja wa kigeni kwa kuwatafutia “wasichana” wa kulala nao usiku. Angefanya nini?

Sebastian aliamua kumkumbusha mkubwa wa kazi maoni yake ya Biblia kuhusu uasherati. Muda si muda, ilikuwa wazi kwamba Sebastian hangeendelea kufanya kazi katika mazingira hayo na kwamba, mwishowe ingembidi kuacha kazi hiyo. Alipata kazi nyingine yenye mshahara mdogo lakini isiyo na vishawishi kama hivyo. Sasa ana dhamiri safi.

Ungefanya nini kama mtu angekulazimisha kufanya au kufumbia macho uasherati? Je, ungekuwa tayari kufanya mabadiliko makubwa? Hivyo ndivyo, Yosefu wa kale alivyofanya, kama inavyoonyeshwa katika Mwanzo 39:7-12.