Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unaimarishwa na Neno la Mungu?

Je, Unaimarishwa na Neno la Mungu?

Je, Unaimarishwa na Neno la Mungu?

WEWE hufanya nini unapokabili majaribu? Yesu alipokabili majaribu ya Shetani alikumbuka maandiko yanayofaa nayo yakamsaidia. (Mathayo 4:1-11) Vivyo hivyo, Mfalme Daudi alipokabili majaribu, aliimarishwa na Neno la Mungu. Alisema: “Fikira zangu zinazofadhaisha zilipokuwa nyingi ndani yangu, faraja zako mwenyewe zilianza kuikumbatia nafsi yangu.”—Zaburi 94:19.

Vivyo hivyo, tunaweza kupata faraja na nguvu za kukabiliana na majaribu kwa kukumbuka andiko fulani tunalopenda. Kwa mfano, Rex, ambaye sasa ana umri wa miaka 89 amekuwa mhudumu wa wakati wote tangu mwaka wa 1931. Lakini anasema: “Mara nyingi nilihisi kuwa sifai nilipopewa mgawo fulani wa pekee katika huduma.” Alikabilianaje na hali hiyo? “Nilikumbuka andiko ninalolipenda la Methali 3:5 ambalo husema: ‘Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe.’ Kukumbuka na kutumia andiko hilo kulinisaidia kutimiza migawo yangu kwa mafanikio.”

Hata vijana hunufaika kwa kukumbuka andiko fulani wanalolipenda. Jack, mwenye umri wa miaka sita anasema kwamba andiko analolipenda ni Mathayo 24:14. Andiko hilo humchochea aende kuhubiri pamoja na wazazi wake. Anasema: “Ninapenda kwenda kuhubiri kila Jumamosi pamoja na mama, baba, na dada yangu.”

Kama Yesu, je, nyakati nyingine wewe hukabili majaribu ya moja kwa moja ya imani? Basi, andiko la Wafilipi 4:13 linaweza kuwa mojawapo ya maandiko unayoyapenda. Kama Mfalme Daudi, je, wewe husumbuliwa na ‘fikira zinazofadhaisha’? Basi unaweza kukabiliana na hali hiyo kwa kukumbuka andiko la Wafilipi 4:6, 7. Je, nyakati nyingine unaogopa kwamba unamtumikia Mungu bure? Basi unaweza kupata nguvu kwa kukumbuka andiko la 1 Wakorintho 15:58.

Kwa kukumbuka maandiko yanayofaa, tunaruhusu Neno la Mungu liwe na nguvu katika maisha yetu. (Waebrania 4:12) Maandiko hayo tunayoyapenda yanaweza kutuimarisha na kutufariji.—Waroma 15:4.