Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

‘Vuka Uingie Utusaidie’

‘Vuka Uingie Utusaidie’

Ripoti ya Watangazaji wa Ufalme

‘Vuka Uingie Utusaidie’

MNAMO Julai 2000, mwito ulitolewa kwa Mashahidi wanaozungumza Kijerumani katika nchi za Austria, Ujerumani, na Uswisi, wahamie Bolivia. Kwa nini? Kwa sababu katika jamii za wakulima wanaoishi katika eneo lenye ukubwa wa kilometa 300 la Santa Cruz, Bolivia, wafuasi wa Menno wanaozungumza Kijerumani walikuwa wanapendezwa na Biblia.

Mashahidi wapatao 140 walikubali mwito huo. Baadhi yao walienda kwa majuma machache, wengine kwa mwaka mmoja au zaidi. Kwa kufanya hivyo, walionyesha roho kama ile iliyoonyeshwa na wamishonari wa karne ya kwanza waliokubali mwito huu: “Vuka uingie Makedonia utusaidie.”—Matendo 16:9, 10.

Inakuwaje kuhubiri katika eneo hilo? Mzee mmoja wa kutaniko la huko anaeleza: “Ili kufikia mojawapo ya jamii 43 za wafuasi wa Menno inakubidi usafiri kwa muda wa saa nane katika barabara za mchanga ukitumia gari lenye kwenda kwa magurudumu yote manne. Ili kufikia maeneo yaliyo mbali zaidi, mara nyingi unaweza kusafiri kwa siku nne na kulala kwenye mahema siku kadhaa. Lakini bila shaka jitihada hiyo inafaa kwa kuwa watu hao hawakuwahi kamwe kusikia habari njema.”

Hapo mwanzoni, wafuasi wengi wa Menno hawakufurahia kutembelewa. Lakini kwa kutembelewa tena na tena wamefahamu ujumbe wa Mashahidi. Kwa mfano, mkulima mmoja alisema kwamba alikuwa akisoma gazeti Amkeni! kwa mwaka mmoja. Kisha akaongeza: “Ninajua kwamba watu wengi hapa hawakubali mambo mnayosema, lakini ninaamini hayo ni kweli.” Katika jamii nyingine, mtu fulani alisema: “Baadhi ya majirani wangu husema kwamba ninyi ni manabii wa uwongo, wengine husema ninyi mna ukweli. Nataka kujichunguzia mwenyewe.”

Sasa kuna kutaniko la Kijerumani nchini Bolivia lenye wahubiri 35, kutia ndani waeneza-injili 14 wa wakati wote. Hadi sasa, watu 14 waliokuwa wafuasi wa Menno wamekuwa watangazaji wa Ufalme, na wengine 9 huhudhuria mikutano kwa ukawaida. Mwanamume mmoja mzee ambaye alibatizwa hivi karibuni alisema: “Tunaona mwongozo wa Yehova waziwazi. Amewatuma ndugu na dada wenye uzoefu ambao huzungumza Kijerumani ili watusaidie. Tunashukuru sana.” Binti yake mwenye umri wa miaka 17, ambaye pia amebatizwa aliongeza kusema: “Shauku ya ndugu na dada wachanga ambao wamekuja ni yenye kuenea. Wengi wao ni mapainia ambao hutumia wakati na pesa zao kuwasaidia wengine. Hilo hufanya nitamani kuwaiga.”

Kwa kweli, wale waliojitahidi ‘kuvuka na kuingia’ ili kusaidia wanapata shangwe na uradhi mwingi.