Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Sala Zako Zinaweza Kubadili Hali?

Je, Sala Zako Zinaweza Kubadili Hali?

Je, Sala Zako Zinaweza Kubadili Hali?

SISI sote kwa wakati fulani tumewahi kukabili hali ngumu ambazo hatungeweza kudhibiti. Biblia inaonyesha kuwa mtume Paulo alijua kwamba sala inaweza kusaidia katika hali ngumu kama hizo.

Alipotiwa gerezani isivyo haki huko Roma, Paulo aliomba waamini wenzake wasali kwa ajili yake, naye akaongeza: “Ninawahimiza ninyi zaidi hasa mfanye hivyo, ili nirudishwe kwenu upesi inavyowezekana.” (Waebrania 13:18, 19) Katika pindi nyingine, Paulo alionyesha uhakika kwamba Mungu angejibu sala ili afunguliwe upesi. (Filemoni 22) Naye alifunguliwa haraka na kuendelea tena na kazi yake ya umishonari.

Lakini, je, kwa kweli sala inaweza kubadili hali yako? Labda. Ingawa hivyo, kumbuka kwamba sala si desturi tu ya kidini. Ni mawasiliano halisi pamoja na Baba yetu wa mbinguni mwenye nguvu zote na mwenye upendo. Tunapaswa kujihisi huru kusema mambo waziwazi katika sala zetu lakini tungoje kwa subira kuona jinsi Yehova atakavyojibu.

Huenda Mungu asijibu kila sala moja kwa moja, ama huenda sikuzote akajibu kwa njia au kwa wakati ambao hatutarajii. Kwa mfano, Paulo alisali mara nyingi kuhusu ‘mwiba wake katika mwili.’ Mungu hakuondoa tatizo la Paulo, liwe lilikuwa gani, lakini alimfariji Paulo kwa maneno haya yenye kuimarisha: “Fadhili zangu zisizostahiliwa zinakutosha wewe; kwa maana nguvu zangu zinakamilishwa katika udhaifu.”—2 Wakorintho 12:7-9.

Sisi pia tunaweza kuwa na hakika kwamba hata ikiwa Mungu haondoi tatizo fulani, anaweza ‘kuifanya njia ya kutokea kusudi tuweze kulivumilia.’ (1 Wakorintho 10:13) Hivi karibuni, Mungu ataondoa mateso yote ya wanadamu. Wakati huu, kumwendea “msikiaji wa sala” kunaweza kubadili hali.—Zaburi 65:2.