Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kufuatia Zaidi Vitu vya Kimwili

Kufuatia Zaidi Vitu vya Kimwili

Kufuatia Zaidi Vitu vya Kimwili

“Ikiwa sikuzote tunatamani kuwa na vitu vingi zaidi, hatutatosheka kamwe.”—Ripoti ya taasisi iitwayo Worldwatch Institute.

“TUNATAKA nini? Kila kitu. Lini? Sasa.” Maneno hayo yalitumiwa sana na baadhi ya wanafunzi wa chuo miaka ya 1960. Huenda leo watu wasisikie hasa maneno hayo, lakini wazo la msingi limebaki. Kwa kweli, inaonekana kwamba kufuatia zaidi vitu vya kimwili kumekuwa jambo muhimu katika wakati wetu.

Kwa watu wengi, kupata mali kumekuwa mojawapo ya jambo kuu zaidi maishani. Aliyekuwa Rais wa Marekani, Jimmy Carter alisema hivi wakati mmoja: “Watu hawatambuliwi tena kwa mambo wanayofanya, bali kwa vitu walivyo navyo.” Je, kuna kanuni zenye thamani zaidi kuliko mali zetu? Ikiwa zipo, ni kanuni gani hizo, nazo zinaweza kuwa na manufaa gani?