Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

‘Nafurahia Mazoezi Niliyopata’

‘Nafurahia Mazoezi Niliyopata’

‘Nafurahia Mazoezi Niliyopata’

KAZUNA mwenye umri mdogo alishangaa mwalimu wake alipomwambia ashiriki katika mashindano ambayo angetoa hotuba katika Kiingereza. Maonyesho hayo yangehusisha shule zote za sekondari katika kisiwa kikubwa cha Hokkaido kilicho kaskazini mwa Japani. Shule yao haikuwahi kuwakilishwa katika mashindano hayo. Kazuna alikuwa na wasiwasi siku ya mashindano hayo kwa kuwa angeshindana na wanafunzi wengine 50 hivi. Alikuwa na wasiwasi hata zaidi alipoona waamuzi wawili ambao lugha yao ya asili ni Kiingereza.

Washindi walitangazwa, kuanzia na yule aliyepokea zawadi ya chini zaidi. Mwishowe, Kazuna alipotangazwa kuwa mshindi, alishangaa. Yeye na mwalimu wake ambaye alikuwa ameketi kando yake, walitazamana kwa mshangao. Akiwa bado ameshtuka, Kazuna alienda jukwaani na kupokea tuzo yake ya ushindi, yaani, zawadi ya kwanza!

“Nilifanikiwa kushinda kwa sababu ya mazoezi yanayoandaliwa na tengenezo la Yehova kupitia Shule ya Huduma ya Kitheokrasi,” akasema Kazuna mwenye furaha. “Ninafurahi sana kwa kupokea mazoezi hayo.” Shule hiyo, ambayo Kazuna alijiandikisha tangu alipokuwa mdogo ni mojawapo ya mikutano ya kutaniko ya Mashahidi wa Yehova. Alipokuwa akijitayarisha kwa ajili ya shindano hilo, Kazuna alizingatia hasa jinsi ya kutumia kikuza-sauti, kuzungumza kwa uchangamfu na shauku, kutumia ishara, kuwatazama wasikilizaji, na masomo mengine yanayofundishwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.

Tunakualika uhudhurie shule hiyo inayofanywa kila juma kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova lililo karibu na kwenu. Jionee mwenyewe jinsi vijana kwa wazee wanavyonufaika. Watu wote wanakaribishwa kwenye mkutano huo. Ili kupata habari zaidi kuhusu shule inayofanywa karibu na nyumbani kwako, tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova katika eneo lenu.