Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wakati wa Chakula Si Wakati wa Kula Tu!

Wakati wa Chakula Si Wakati wa Kula Tu!

Wakati wa Chakula Si Wakati wa Kula Tu!

KILA mtu hufurahia chakula kitamu. Chakula hufurahisha hata zaidi na kutosheleza mengi zaidi ya njaa yetu tunapokuwa na mazungumzo yenye kujenga na ushirika pamoja na watu tunaowapenda. Familia nyingi huwa na zoea la kula pamoja angalau mara moja kwa siku. Wakati wa chakula, familia hupata nafasi ya kuzungumzia matukio au mipango ya siku hiyo. Wazazi ambao huwasikiliza watoto wao pindi hiyo, huelewa kwa kiasi fulani jinsi watoto hao wanavyofikiri na kuhisi. Baada ya muda, ushirika wenye kufurahisha na kustarehesha unaofurahiwa wakati wa chakula hufanya washiriki wa familia wawe na usalama, watumainiane, na wapendane na hivyo kufanya familia kuwa imara.

Leo, washiriki wengi wa familia hawapati nafasi ya kula pamoja kwa sababu wana shughuli nyingi. Katika sehemu fulani ulimwenguni, kula pamoja kama familia au hata kuzungumza wakati wa chakula huonwa kuwa jambo lisilofaa. Familia nyingine huwa na zoea la kufungua televisheni wakati wa chakula, na hilo hufanya wakose nafasi ya kuwa na mazungumzo muhimu.

Hata hivyo, wazazi Wakristo huwa macho sikuzote kutafuta nafasi ya kujenga familia zao. (Methali 24:27) Zamani, wazazi waliambiwa kwamba mojawapo ya njia zenye matokeo zaidi za kuwafundisha watoto wao Neno la Mungu ni wakati ‘wanapoketi katika nyumba zao.’ (Kumbukumbu la Torati 6:7) Kula pamoja na watoto wao kwa ukawaida huwapa wazazi nafasi ya pekee ya kusitawisha katika watoto wao upendo kwa Yehova na kanuni zake adilifu. Kukiwa na mazingira yenye kustarehesha na kufurahisha, familia yako itafurahia na kujengwa wakati wa chakula. Naam, fanya wakati wa chakula usiwe wakati wa kula tu!