Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jinsi ya Kutumia Kila Siku kwa Hekima

Jinsi ya Kutumia Kila Siku kwa Hekima

Jinsi ya Kutumia Kila Siku kwa Hekima

“UTUONYESHE jinsi ya kuzihesabu siku zetu hivi kwamba tupate kuuingiza moyo wa hekima.” (Zaburi 90:12) Hivyo ndivyo Musa, mwandikaji wa Biblia, alivyosali kwa unyenyekevu. Alikuwa akiomba nini hasa? Je, sisi pia tunapaswa kutoa sala kama hiyo?

Katika mstari wa 10, Musa anataja kwa masikitiko ufupi wa maisha ya mwanadamu. Pindi nyingine, Musa aliandika maneno haya ya Ayubu: “Mwanadamu, aliyezaliwa na mwanamke, ana maisha mafupi na yenye kujaa msukosuko.” (Ayubu 14:1) Ni wazi kwamba Musa alijua maisha ya mwanadamu asiye mkamilifu ni mafupi. Hivyo, aliona kila siku ya maisha yake kuwa muhimu sana. Kwa kusali hivyo kwa Mungu, Musa alionyesha kwamba anatamani kutumia siku zilizobaki za maisha yake kwa hekima, yaani, kwa njia ambayo itampendeza Muumba wake. Je, sisi pia hatupaswi kujitahidi kutumia kila siku ya maisha yetu vizuri? Ikiwa tunataka kukubaliwa na Mungu sasa, tutajitahidi kufanya hivyo.

Kuna jambo lingine lililowachochea Musa na Ayubu, nalo linapaswa kutuchochea pia. Watu hao wawili walitazamia kupata thawabu wakati ujao, yaani, kuishi duniani katika hali nzuri. (Ayubu 14:14, 15; Waebrania 11:26) Wakati huo, kazi nzuri za wanadamu hazitakatishwa na kifo. Muumba wetu anakusudia waaminifu waishi milele katika dunia iliyo paradiso. (Isaya 65:21-24; Ufunuo 21:3, 4) Unaweza kuwa na tumaini hilo ‘ukihesabu siku zako ili upate kuuingiza moyo wa hekima.’