Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Msiba Watokea Ghafula

Msiba Watokea Ghafula

Msiba Watokea Ghafula

OWEN, mvulana mwenye umri wa miaka miwili na nusu, alikuwa akicheza katika bafu nyumbani kwao. Alipanda na kuifikia kabati ya dawa ambayo wazazi wake walifikiri hawezi kuifikia. Owen aliona chupa iliyomvutia kati ya vitu vilivyokuwa ndani ya kabati hiyo. Alipoifungua na kunywa umajimaji uliokuwa ndani, msiba ulitokea.

Chupa hiyo ilikuwa na asidi kali, na kwa kusikitisha, Owen alikufa. Wazazi wake walihuzunika sana. Percy, baba yake, alienda kwa kasisi wa kanisa lake ili kufarijiwa. Alimwuliza, “Kwa nini jambo hili lilitukia?” Kasisi huyo akamjibu, “Mungu alitaka malaika mwingine mdogo mbinguni.” Mzazi huyo mwenye huzuni nyingi alihisi kwamba Mungu hakutenda haki hata kidogo. Je, kweli Mungu alitaka msiba huo utokee? Kwa kukata tamaa, Percy aliamua kuliacha kanisa hilo.

Alipofikiria yaliyotokea, Percy alijiuliza: ‘Je, mtoto wangu bado anateseka? Je, nitamwona tena?’

Huenda hata wewe hujui ni nini hutokea mtu anapokufa, na ikiwa wakati ujao itawezekana kuungana na wapendwa wetu waliokufa. Neno la Mungu, Biblia, hujibu maswali hayo. Biblia ina majibu yaliyo wazi na yenye kuwafariji wote waliofiwa. Isitoshe, inafunua tumaini tukufu ambalo Mungu ameahidi, yaani, ufufuo.

Tafadhali soma makala inayofuata ili upate kujua mengi zaidi kuhusu tumaini hilo zuri.