Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Wewe Huzungumza na Wapendwa Wako?

Je, Wewe Huzungumza na Wapendwa Wako?

Je, Wewe Huzungumza na Wapendwa Wako?

“UWEZO wetu wa kuwasiliana na wapendwa wetu unaendelea kupungua sana,” laripoti gazeti Polityka la Poland. Huko Marekani, inakadiriwa kwamba wenzi wa ndoa hutumia dakika sita tu kwa siku kuzungumza pamoja kwa njia yenye kujenga. Wataalamu fulani wanafikiri kwamba nusu ya visa vya kutengana na kutalikiana vinasababishwa na hali hiyo.

Namna gani mazungumzo kati ya wazazi na watoto wao? Mara nyingi, “mazungumzo kati ya wazazi na watoto huwa kama mahojiano: Ilikuwaje shuleni? Rafiki zako wakoje?” inasema ripoti hiyo. Pia inauliza: “Watoto wetu watawezaje kujifunza kusitawisha urafiki wa karibu?”

Kwa kuwa mawasiliano mazuri hayawezi kuwepo bila jitihada yoyote, tunawezaje kuboresha uwezo wetu wa kuzungumza? Mwanafunzi Mkristo Yakobo alitutolea shauri hili muhimu: “Kila mtu lazima awe mwepesi kuhusu kusikia, si mwepesi wa kusema, si mwepesi wa ghadhabu.” (Yakobo 1:19) Naam, ili kuwa na mazungumzo yenye kujenga tunahitaji kusikiliza kwa makini bila kumkatiza mtu au kufikia uamuzi wa haraka bila kufikiria. Tuepuke kuwachambua-chambua watu kwa sababu kufanya hivyo kunaweza kukatiza mazungumzo. Isitoshe, Yesu alitumia maswali ya busara, si ili kuwahoji wasikilizaji wake, bali kujua yale yaliyokuwa moyoni mwao na hivyo kuimarisha urafiki kati yake na wasikilizaji hao.—Methali 20:5; Mathayo 16:13-17; 17:24-27.

Kwa kutumia kanuni nzuri zinazopatikana katika Biblia, anzisha mazungumzo na uwasiliane na wapendwa wako. Huenda hilo likafanya mwe na uhusiano mchangamfu ambao mtafurahia kwa miaka mingi au hata maisha yenu yote.