Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Upendezi Katika Biblia Unathaminiwa

Upendezi Katika Biblia Unathaminiwa

Upendezi Katika Biblia Unathaminiwa

MARIANNA, ambaye ni Shahidi wa Yehova kusini mwa Italia, ana umri wa miaka 18 na yuko katika mwaka wake wa mwisho wa shule ya sekondari. Yuko katika shule moja na baadhi ya vijana Mashahidi.

Marianna anaandika hivi: “Kwa miaka kadhaa sasa, wengine wetu tumekuwa tukisoma andiko la siku kutoka katika kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku wakati wa mapumziko ya shule. Tungeweza tu kusomea andiko hilo katika kimojawapo cha vijia vilivyo karibu na chumba cha walimu. Mahali hapo hapakuwa na utulivu Wengi wa walimu waliopita hapo walituona, na baadhi yao walisimama kuona tulichokuwa tukifanya. Mara nyingi hilo lilitupa nafasi ya kujibu maswali yao. Kwa wastani, kila siku mwalimu mmoja alisimama ili kuzungumza nasi. Wengine walisimama ili kusikiliza mazungumzo yetu ya andiko la siku na walivutiwa na upendezi ambao Mashahidi wanaonyesha kuhusu mambo ya kiroho. Pindi fulani, naibu-mkuu wa shule alituruhusu kufanyia mazungumzo yetu katika chumba cha walimu.

“Baada ya kuona mahali tulipokuwa tukizungumzia andiko la siku, mwalimu wetu alimuuliza mkuu wa shule ikiwa tungeweza kuzungumzia andiko la siku katika darasa moja ambalo angalau lilikuwa na utulivu. Mkuu huyo wa shule alikubali, na mwalimu wetu akatusifu mbele ya darasa lote kwa mfano wetu mzuri. Sote tunafurahia sana pendeleo hilo kubwa ambalo Yehova ametupatia.”