Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wanawahubiria Viziwi Habari Njema

Wanawahubiria Viziwi Habari Njema

Wanawahubiria Viziwi Habari Njema

“WANAWALETEA mambo ya kiroho!” Hivyo ndivyo msimamizi wa kituo cha kuwatunzia wazee huko Navalcarnero, Madrid, Hispania, alivyosema hivi karibuni kuhusu ziara za Mashahidi wa Yehova kwenye kituo chake. Kwa nini alisema hivyo?

Baadhi ya wakaaji wa kituo cha Rosas del Camino ni viziwi. Hata hivyo, kwa kuwa Mashahidi wamejitahidi kujifunza Lugha ya Ishara ya Kihispania, wanaweza kuwasiliana na wakaaji hao. Msimamizi huyo aliwasifu Mashahidi kwa kukubali kuwafundisha watu walio na uhitaji wa kiroho bila malipo. Alitaja matokeo mazuri ambayo yametokana na kuwafundisha wakaaji wa kituo hicho habari njema ya Ufalme. Pia, wakaaji wa kituo hicho, hasa wale wenye matatizo ya kusikia au ya kuona, huthamini sana wanapotembelewa na Mashahidi.

Sasa, Eulogio, mmoja wa wakaaji hao ambaye ni kipofu na kiziwi, anajifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Siku moja, wakati ambapo funzo lilikuwa likiendelea, mzee mmoja alikaribia na kumpa Shahidi huyo shairi ambalo wakaaji wa kituo hicho walitunga ili kutoa shukrani. Shairi hilo lilikuwa na kichwa hiki: “Maisha ya Shahidi.” Lilisema hivi kwa sehemu: “Wanaishi maisha mazuri, wakiwa na mwenendo mzuri, nao wanapata hekima na shangwe kutoka kwa Yehova. Wao hutembelea nyumba za watu mara nyingi kwa sababu wanamtegemea Yehova.”

Kumtegemea Yehova kumewasaidia Mashahidi wengi ulimwenguni pote kujifunza lugha ya ishara ya viziwi wa nchi yao. Kwa kufanya hivyo, wanazungumza na watu hao ujumbe wa tumaini wenye kutia moyo unaopatikana katika Biblia.