Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Kweli Kuna Ibilisi?

Je, Kweli Kuna Ibilisi?

Je, Kweli Kuna Ibilisi?

UNA maoni gani kumhusu Ibilisi? Je, unafikiri kwamba yeye ni kiumbe halisi anayewashawishi watu watende mambo maovu, au je, unafikiri Ibilisi ni uovu tu? Je, Ibilisi ni kiumbe anayepaswa kuogopwa, au je, anapaswa kuonwa kuwa jambo la kuwaziwa la ushirikina au kiumbe anayetajwa katika hadithi tu? Je, neno “ibilisi” linamaanisha nguvu fulani zisizoonekana katika ulimwengu ambazo zinasababisha uharibifu? Je, neno hilo linaweza tu kumaanisha tabia mbovu za wanadamu, kama vile wanatheolojia wengi wa siku hizi wanavyodai?

Haishangazi kwamba wanadamu wana maoni tofauti kuhusu Ibilisi. Fikiria jinsi inavyoweza kuwa vigumu kumtambua mtu anayejua sana kujigeuza ili asijulikane! Inakuwa vigumu hasa ikiwa mtu huyo ameazimia kuficha jinsi alivyo. Biblia inaeleza kwamba Ibilisi ni kiumbe wa namna hiyo. Ikimtaja Ibilisi kuwa Shetani, Biblia inasema hivi: “Shetani mwenyewe huendelea kujigeuza mwenyewe kuwa malaika wa nuru.” (2 Wakorintho 11:14) Ingawa yeye ni mwovu, Ibilisi hujidai kuwa kiumbe mzuri ili awadanganye wengine. Na akifanikiwa kuwafanya watu waamini kwamba hakuna Ibilisi, kusudi lake hufanikiwa hata zaidi.

Hivyo basi, Ibilisi ni nani? Alitokea lini na jinsi gani? Anawashawishije wanadamu leo? Je, kuna jambo tunaloweza kufanya ili kupinga uvutano wake? Biblia ina masimulizi sahihi kuhusu Ibilisi tangu wakati alipoanza, nayo inatoa majibu sahihi kwa maswali hayo.

[Picha katika ukurasa wa 3]

Inaweza kuwa vigumu kumtambua mtu ambaye ameazimia kuficha jinsi alivyo!