Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umefurahia kusoma matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona kama unaweza kujibu maswali yafuatayo:

Kwa nini dhambi ya kwanza, yaani, kutotii kwa Adamu, inaweza kulinganishwa na ugonjwa unaorithiwa?

Ni kama ugonjwa kwa sababu wazao wa Adamu walirithi dhambi kutoka kwake. Hivyo, tumerithi dosari ya dhambi, kama vile watoto fulani hurithi ugonjwa kutoka kwa wazazi wao.—8/15, ukurasa wa 5.

Ni mambo gani yanayosababisha ongezeko la jeuri leo?

Shetani anajaribu kuwafanya watu wamkasirishe Yehova kwa kuingiza roho ya jeuri katika mioyo yao. Yeye hutumia vitu kama vile sinema, muziki, na michezo ya kompyuta ambayo huhusisha ukatili mkubwa sana na mauaji. Jeuri kwenye vyombo vya habari imechangia matendo mengi ya jeuri.—9/1, ukurasa wa 29.

Pontio Pilato alikuwa nani?

Alikuwa Mroma wa cheo cha chini ambaye yaelekea alikuwa katika jeshi. Maliki Mroma Tiberio alimtawaza Pilato kuwa gavana wa mkoa wa Yudea mwaka wa 26 W.K. Wakati wa kusikiliza kesi dhidi ya Yesu, Pilato alisikiliza mashtaka ya viongozi Wayahudi. Ili kuupendeza umati, alikubali Yesu auawe.—9/15, ukurasa wa 10-12.

Ni nini ile “ishara” inayotajwa kwenye Mathayo 24:3?

Ishara hiyo ina sehemu nyingi. Ishara hiyo inatia ndani vita, njaa, tauni, na matetemeko ya nchi, na ingewawezesha wafuasi wa Yesu kutambua “kuwapo” kwake na pia “umalizio wa mfumo wa mambo.”—10/1, ukurasa wa 4-5.

Vituo vikuu vya Wayahudi walioishi nje ya Palestina vilikuwa gani?

Katika karne ya kwanza, vituo vikuu vya Wayahudi vilikuwa Siria, Asia Ndogo, Babilonia, na Misri, na kulikuwa na jumuiya ndogo za Wayahudi katika eneo la Ulaya la Milki ya Roma.—10/15, ukurasa wa 12.

Je, Mkristo anaweza kudumisha dhamiri njema akikubali kazi inayohusisha kuwa na silaha?

Kufanya kazi inayohusisha kubeba bunduki au silaha nyingine ni uamuzi wa mtu binafsi. Lakini kazi kama hiyo humfanya mtu akabili uwezekano wa kuwa na hatia ya damu anapotumia silaha hiyo au kukabili hatari ya kujeruhiwa au kuuawa anaposhambuliwa au mtu anapolipiza kisasi. Mkristo anayebeba silaha hawezi kustahili kupata mapendeleo yoyote ya pekee kutanikoni. (1 Timotheo 3:3, 10)—11/1, ukurasa wa 31.

Kwa kuwa neno “Har–Magedoni” linatokana na usemi “Mlima wa Megido,” je, vita vya Har-Magedoni vitapiganwa kwenye mlima huko Mashariki ya Kati?

La. Hakuna Mlima wa Megido. Badala yake, kuna kilima tu kando ya bonde fulani huko Israeli. Eneo hilo haliwezi kuwatosha “wafalme [wote] wa dunia na majeshi yao.” Vita vikuu vya Mungu vitapiganwa duniani pote, navyo vitakomesha vita vyote. (Ufunuo 16:14, 16; 19:19; Zaburi 46:8, 9)—12/1, ukurasa wa 4-7.