Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Wewe Ni Kama Mti wa Lagani Auna?

Je, Wewe Ni Kama Mti wa Lagani Auna?

Je, Wewe Ni Kama Mti wa Lagani Auna?

KATIKA kijiji kimoja nje ya Bandari ya Moresby, Papua New Guinea, wahudumu wawili walikuwa wakirudi nyumbani kutoka katika kazi ya kuhubiri. Walipokuwa wakitembea, waliona mti maridadi. Aliyekuwa mzee kwa umri akasema: “Ah, ona lagani auna!” Akimgeukia mhudumu kijana, aliendelea kusema hivi: “Jina hilo linamaanisha ‘mti wa kila mwaka.’ Tofauti na miti mingi ya nchi za joto, kila mwaka mti huo huangusha majani yake na huonekana kuwa umekauka. Hata hivyo, mvua inaponyesha, mti huu huchipua maua na kuwa maridadi tena.”

Tunaweza kujifunza jambo fulani kutokana na mti wa lagani auna, kama unavyojulikana. Kulingana na wataalamu fulani, mti huo ni miongoni mwa miti mitano maridadi zaidi ulimwenguni ambayo huchipua maua. Ingawa unapoteza maua na majani yake wakati wa kiangazi, mti huo huhifadhi maji. Mizizi yake ni yenye nguvu na inaweza kukua kwenye miamba iliyo chini ya ardhi. Kupitia mizizi hiyo, mti huo hustahimili upepo mkali. Kwa ufupi, mti huo unasitawi kwa kujipatanisha na hali ngumu zaidi.

Huenda tukajikuta katika hali ambazo zinajaribu ubora wa imani yetu. Ni nini kitakachotusaidia kuvumilia? Kama mti wa lagani auna, tunaweza kunywa na kuhifadhi maji ya Neno la Mungu yanayotoa uzima. Tunapaswa pia kushikamana kabisa na ‘mwamba wetu,’ Yehova, na pia tengenezo lake. (2 Samweli 22:3) Kwa kweli, mti wa lagani auna unatukumbusha vizuri kwamba hata katika hali ngumu, tunaweza kudumisha nguvu za kiroho na uzuri wetu ikiwa tutafaidika na msaada ambao Yehova anatutolea. Kwa kufanya hivyo, ‘tutarithi ahadi’ ambazo ametutolea, kutia ndani ahadi ya uzima wa milele.—Waebrania 6:12; Ufunuo 21:4.