Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mungu Ana Kusudi Gani Kuelekea Dunia?

Mungu Ana Kusudi Gani Kuelekea Dunia?

Mungu Ana Kusudi Gani Kuelekea Dunia?

KWA nini wewe hufurahia kutembea au kupunga hewa katika bustani iliyo na maua yenye harufu tamu? Kwa nini wewe husisimuka unapoona ziwa lenye kupendeza au milima mirefu yenye vilele mawinguni? Kwa nini wewe hufurahia kusikiliza sauti tamu ya ndege juu ya miti? Na kwa nini inapendeza kuona swara akirukaruka kwa madaha au kundi la kondoo wakiwa malishoni?

Jibu la maswali hayo ni moja. Tuliumbwa tuishi katika Paradiso! Mwanzoni, wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Hawa, waliishi katika paradiso. Tulirithi tamaa ya kuishi katika Paradiso kutoka kwao. Nao walipata tamaa hiyo kutoka kwa Muumba wao, Yehova Mungu. Alijua kwamba tutafurahia kuishi katika Paradiso kwa kuwa alituumba tukiwa na sifa zinazotuwezesha kufurahia makao haya mazuri ya kidunia.

Kwa nini Yehova aliiumba dunia? “Aliiumba ili ikaliwe” na wanadamu. (Isaya 45:18) “Mtengenezaji wa dunia” aliwapa Adamu na Hawa makao mazuri yaliyokuwa paradiso, yaani, bustani ya Edeni. (Yeremia 10:12; Mwanzo 2:7-9, 15, 21, 22) Haikosi walifurahia mito, maua, na miti iliyokuwa humo! Bustani hiyo ilikuwa na ndege wenye kuvutia, na wanyama wa kila aina. Wote hao hawakuwa tisho kwa wanadamu. Samaki na viumbe wengine waliogelea katika maji safi ya dunia. Zaidi ya hayo, Adamu na Hawa waliishi pamoja. Wangeweza kupata watoto, kupanua Paradiso, na kufurahia ushirika wa familia yao yenye shangwe iliyokuwa ikizidi kukua.

Ingawa dunia si paradiso leo, tunaweza kuilinganisha na makao mazuri ya familia yenye furaha. Makao yetu tuliyopewa na Mungu yana vitu tunavyohitaji kama vile, mwangaza, joto, maji, na chakula. Tunathamini sana mbalamwezi wakati wa usiku na mwangaza na joto kutoka kwa jua wakati wa mchana! (Mwanzo 1:14-18) Katika dunia kuna makaa na mafuta tunayoweza kutumia. Tunapata maji kutokana na mvua, mito, maziwa, na bahari. Dunia imefunikwa kwa nyasi za kijani kibichi zilizo kama zulia.

Kama vile chakula kinavyoweza kuhifadhiwa ghalani, kuna chakula tele duniani. Kupitia mimea ya chakula na matunda shambani, Yehova ‘hutupa majira yenye kuzaa matunda, akijaza mioyo yetu kwa chakula na uchangamfu.’ (Matendo 14:16, 17) Kwa kuwa tayari dunia ni mahali pazuri hivyo, wazia jinsi itakavyokuwa wakati ambapo “Mungu mwenye furaha,” Yehova, atakapoifanya kuwa paradiso!—1 Timotheo 1:11.

[Picha katika ukurawa wa 2 zimeandaliwa na]

COVER: Earth: NASA photo; Stars: NASA, ESA and AURA/Caltech