Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Shati la Manyoya na Hali ya Kiroho

Shati la Manyoya na Hali ya Kiroho

Shati la Manyoya na Hali ya Kiroho

MFALME LOUIS wa 9 wa Ufaransa alikuwa akivaa shati la manyoya. Kwa msaada wa shati hilo, Sir Thomas More alipokuwa kijana alikesha kwa saa 19 au 20 kila siku kwa miezi kadhaa akijifunza sheria. Inajulikana kwamba More alivaa shati kama hilo karibu maisha yake yote. Wakati Thomas Becket, Askofu Mkuu wa Canterbury, alipouawa katika Kanisa Kuu la Canterbury, shati moja kama hilo lilipatikana bila kutazamiwa chini ya mavazi yake. Watu hao wa zamani walifanana kwa njia gani? Walitesa miili yao kwa kutumia shati la manyoya.

Shati hilo la manyoya lilikuwa vazi lenye kukwaruza lililotengenezwa kwa manyoya ya mbuzi. Liliwekwa karibu na ngozi ili kuiwasha na kuikwaruza na kusababisha uchungu mwingi. Pia, lilivutia chawa. Inasemekana kwamba Thomas Becket, alivaa shati hilo la manyoya pamoja na nguo za ndani zilizotengenezwa kwa manyoya, mpaka “shati hilo likajaa chawa.” Baada ya karne ya 16, badala ya kuvaa mashati ya manyoya ya mbuzi, watu walianza kuvaa mashati yaliyotengenezwa kwa seng’enge badala ya manyoya ya mbuzi. Watu waliovaa mashati hayo waliumia sana.

Kulingana na kamusi moja, kusudi la shati hilo la manyoya, sawa na vitu vingine vinavyotumiwa kujitia nidhamu, ni “kuudhibiti mwili wenye dhambi na hivyo kusitawisha mtazamo wa kiroho na njia nzuri ya maisha.” Mbali na watu waliojinyima raha kabisa, watu ambao hawakuwa wanadini, kutia ndani watu wenye mamlaka serikalini, walivaa shati hilo. Hata leo dini fulani hutumia mashati hayo.

Je, kuvaa shati la manyoya au kujinyima mahitaji ya kimwili kunamfanya mtu awe na hali nzuri ya kiroho? La, hali nzuri ya kiroho haitegemei mazoea kama hayo. Hata mtume Paulo alipinga mazoea ya “kuutendea mwili kwa ukali.” (Wakolosai 2:23) * Badala yake, ili kuwa na hali nzuri ya kiroho, tunapaswa kupata ujuzi juu ya Mungu kwa kujifunza kwa bidii Neno lake na kuutumia ujuzi huo maishani.

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 5 Ili kupata habari zaidi kuhusu jambo hilo, ona gazeti la Amkeni! la Oktoba 8, 1997, “Maoni ya Biblia: Je, Kujinyima Sana Raha na Anasa Ndio Ufunguo wa Kupata Hekima?

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

King Louis IX, top: From the book Great Men and Famous Women; Thomas Becket, center: From the book Ridpath’s History of the World (Vol. IV); Thomas More, bottom: From the book Heroes of the Reformation, 1904