Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umefurahia kusoma matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona kama unaweza kujibu maswali yafuatayo:

• Kama ilivyotabiriwa katika Zaburi 72:12, Yesu ‘atamkomboaje maskini’?

Wakati wa utawala wake, hakutakuwa na ufisadi, bali kutakuwa na haki kwa wote. Mara nyingi vita husababisha umaskini, lakini Kristo ataleta amani kamilifu. Yeye huwasikitikia watu, naye atawaunganisha watu wote na kuhakikisha kwamba wanadamu wana chakula cha kutosha. (Zaburi 72:4-16)—5/1, ukurasa wa 7.

• Sisi Wakristo tunaweza kutumiaje ‘uhuru wetu wa kusema’? (1 Timotheo 3:13; Filemoni 8; Waebrania 4:16)

Tunaweza kuutumia kwa kuwahubiria wengine kwa bidii na kwa ujasiri, kwa kufundisha na kutoa mashauri haraka na kwa matokeo, na kwa kumweleza Mungu mambo yote yaliyo moyoni mwetu tunaposali, huku tukiwa na uhakika kwamba atasikia na kujibu.—5/15, ukurasa wa 14-16.

• Katika Sheria ya Musa, kwa nini mahusiano fulani ya ngono yalimfanya mtu ‘asiwe safi’?

Sheria zinazohusu uchafu unaosababishwa na kutokwa na shahawa, hedhi, na kuzaa zilisaidia watu wawe safi na kudumisha afya njema, zilikazia utakatifu wa damu, na kuonyesha uhitaji wa upatanisho kwa ajili ya dhambi.—6/1, ukurasa wa 31.

• Ikiwa mtu anataka kuwa na furaha, kwa nini inafaa achunguze kitabu cha Zaburi?

Watungaji wa Zaburi walijua kwamba furaha ya kweli inatokana na kuwa na uhusiano mzuri pamoja na Mungu. (Zaburi 112:1) Walikazia kwamba uhusiano wa kibinadamu, vitu vya kimwili, au mafanikio ya mtu haviwezi kuleta furaha inayotokana na kuwa miongoni mwa “watu ambao Mungu wao ni Yehova.” (Zaburi 144:15)—6/15, ukurasa wa 12.

• Waisraeli wa kale walikuwa na uhusiano gani wa pekee pamoja na Yehova?

Katika mwaka wa 1513 K.W.K., Yehova alianzisha uhusiano mpya pamoja na Waisraeli, yaani, alifanya agano pamoja nao. (Kutoka 19:5, 6; 24:7) Kuanzia wakati huo, Waisraeli walizaliwa wakiwa washiriki wa taifa teule la Mungu lililojiweka wakfu kwake. Hata hivyo, kila Mwisraeli alipaswa kufanya uamuzi wa kibinafsi wa kumtumikia Mungu.—7/1, ukurasa wa 21-22.

• Kwa nini tufanye mambo yote “bila kunung’unika”? (Wafilipi 2:14)

Mifano mingi ya Kimaandiko inaonyesha kwamba manung’uniko yaliwaathiri watu wa Mungu. Tunapaswa kufikiria kwa uzito madhara ambayo yanaweza kutokea leo kwa kunung’unika. Wanadamu wasio wakamilifu wana mwelekeo wa kulalamika, nasi tunapaswa kuwa chonjo kugundua dalili yoyote ya kutaka kulalamika na kuepuka kufanya hivyo.—7/15, ukurasa wa 16-17.

• Tunajuaje kwamba hekima inayofafanuliwa kwenye Methali 8:22-31 si sifa ya hekima tu?

Hekima hiyo ‘ilitokezwa,’ au kuumbwa, ikiwa ndiyo mwanzo wa njia ya Yehova. Mungu amekuwapo na amekuwa mwenye hekima sikuzote; hekima yake haikuumbwa. Hekima inayotajwa katika Methali 8:22-31 ilikuwa kando ya Mungu ikiwa “stadi wa kazi.” Maneno hayo yanamhusu kiumbe wa roho aliyezaliwa na kuwa Yesu ambaye alifanya kazi kwa ukaribu sana pamoja na Mungu katika kazi ya uumbaji. (Wakolosai 1:17; Ufunuo 3:14)—8/1, ukurasa wa 31.