Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kwa Nini Ufanye Yaliyo Sawa?

Kwa Nini Ufanye Yaliyo Sawa?

Kwa Nini Ufanye Yaliyo Sawa?

MWANAMUME mmoja msomi alisema hivi wakati fulani: “Nina uwezo wa kutaka, bali uwezo wa kufanya yaliyo mazuri haupo. Kwa maana lile jema ninalotaka silifanyi, bali lile baya nisilotaka ndilo ninalozoea kulifanya.” Kwa nini haikuwa rahisi kwa mwanamume huyo kufanya mazuri aliyotaka? Alieleza: “Basi, mimi naona sheria hii katika hali yangu: kwamba ninapotaka kufanya yaliyo sawa, yaliyo mabaya yapo pamoja nami. Kwa kweli naipenda sheria ya Mungu kulingana na mtu niliye kwa ndani, lakini mimi naona ndani ya viungo vyangu sheria nyingine ikipigana na sheria ya akili yangu na kunichukua mateka kwa sheria ya dhambi iliyo ndani ya viungo vyangu.”—Waroma 7:18, 19, 21-23.

Maneno hayo ya mtume Paulo yaliyoandikwa karibu miaka 2,000 iliyopita, yanaeleza kwa nini si rahisi kwa wanadamu wasio wakamilifu kufanya yaliyo sawa. Tunahitaji kuwa imara kiadili ili tushikamane na kanuni zinazofaa, hasa tunapokabili majaribu. Hivyo, tunapaswa kujiuliza, Ni sababu gani iliyo muhimu zaidi ya kufanya yaliyo sawa?

Fikiria yale ambayo Maandiko yanasema kuhusu wakati ujao wa mtu ambaye ni mnyoofu kiadili. Tunasoma hivi katika Zaburi 37:37, 38: “Mwangalie mtu asiye na lawama na uendelee kumwangalia mnyoofu, kwa maana wakati ujao wa mtu huyo utakuwa wenye amani. Lakini wakosaji hakika wataangamizwa pamoja; wakati ujao wa watu waovu hakika utakatiliwa mbali.” Andiko la Methali 2:21, 22 linatuambia hivi: “Wanyoofu ndio watakaokaa duniani, na wasio na lawama ndio watakaobaki ndani yake. Nao waovu, watakatiliwa mbali kutoka duniani; nao wenye hila, watang’olewa kutoka ndani yake.”

Ingawa ahadi hizo na nyinginezo zilizo katika Biblia hutuchochea kuendelea kufanya mambo yanayompendeza Mungu, ahadi hizo si sababu muhimu zaidi ya kufanya yaliyo sawa. Sababu muhimu zaidi inahusiana na suala ambalo linahusu viumbe wote wenye akili. Makala inayofuata inazungumzia suala hilo na jinsi linavyotuhusu.